Skip to main content

TOM MBOYA SAUTI YA WANYONGE ILIYOZIMIKA GHAFLA…!!!





Thomas Joseph Odhiambo Mboya (pichani), alikuwa ni mmoja wa waasisi wa Chama cha Kenya African National Union (Kanu)

Wakati anauawa, Tom Mboya, alikuwa ni Waziri wa Mipango ya Uchumi na Maendeleo. Pia alikuwa ni mwanasiasa aliyepewa nafasi kubwa ya kuja kuwa rais wa nchi hiyo baada ya Kenyatta.


Mboya alizaliwa Agosti 15, 1930 huko Kilima Mbogo karibu na Mji wa Thika katika maeneo ambayo wakati ule yalikuwa yanaitwa White Highlands.

Alisoma na kupata elimu ya juu, akaenda Uingereza na kurejea Kenya mwaka 1956 akafanya kazi na kujiunga na siasa. Wakati huo Waingereza walikuwa wanajaribu kulidhibiti wimbi la wapigania uhuru wa Mau Mau, waliokuwa wanataka ardhi yao na uhuru wa Kenya.

Aliajiriwa na Halmashauri ya Jiji la Nairobi, akajiunga na Chama cha Wafanyakazi cha African Staff Association na kuchaguliwa kuwa rais wa chama hicho ambacho kikaitwa Kenya Local Government Workers Union.

Aliingia katika bunge ambalo miongoni mwa wabunge 50, Waafrika walikuwa nane tu.

Katika medani ya kimataifa, akachaguliwa kuwa mwenyekiti wa All-African Peoples Conference nchini Ghana, ambao uliitishwa na Kwame Nkrumah. Wakati huo Mboya alikuwa na umri wa miaka 28 tu.

Mnamo1959, alianzisha mchakato wa kupeleka Waafrika kusoma nchini Marekani, ambapo wanafunzi 81 walihusika.

Juhudi hizo za Mboya zilimfanya Rais John Kennedy wa Marekani mwaka 1960, kujumuisha pia wanafunzi kutoka Uganda, Tanganyika (Tanzania) na Zanzibar, Rhodesia ya Kaskazini (ambayo sasa ni Zambia) Rhodesia ya Kusini (sasa ni Zimbabwe) na Nyasaland ambayo sasa ni Malawi.

Mradi huo uliwezesha wanafunzi 230 wa Afrika kupata masomo nchini Marekani mwaka 1960 ambapo mamia zaidi walifuatia mwaka 1961.

Yote hayo yalizidi kumpa Mboya umaarufu mkubwa machoni mwa umma na akazidi kushika nyadhifa za juu kila kukicha.

Ni katika Mtaa wa Independence Avenue (ambao sasa ni Moi Avenue), mchana wa Julai 5, 1969 ambapo Nashon Isaac Njenga Njoroge alimpiga risasi na kumuua akiwa anatoka katika duka moja la madawa.

Mboya, aliyekuwa na umri wa miaka 39, alikufa papo hapo.

Mboya aliacha mke (Pamela) na watoto watano. Alizikwa katika kaburi maalum kwenye Kisiwa cha Rusinga. Kaburi hilo lilijengwa mnamo mwaka 1970.

Pamela, ambaye baadaye alizaa mtoto mmoja aitwaye Tom Mboya Jr na kaka wa marehemu Tom Mboya aitwaye Alphonce Okuku, naye alikufa mwaka 2009 wakati akitibiwa huko Afrika Kusini.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...