Skip to main content

UMOJA WA MATAIFA WANAWAKE WAZINDUA KUNDI LA ‘HEFORSHE’, LENGO KUWEKA USAWA WA KIJINSIA



Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa hotuba katika mdahalo kuhusu wanawake na uzinduzi wa Kundi la `HeForShe`.

Umoja wa Mataifa Wanawake (UN Women) nchini umefanya uzinduzi wa kundi la mshikamano la Kimataifa linalohusisha wanaume na wavulana lililo na malengo ya kuhakikisha kunapatikana usawa wa kijinsia baina ya wanaume na wanawake ‘HeForShe’.

Akizindua kundi hilo, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez alisema usawa kijinsia ni haki ya kila binadamu na kupitia kundi hilo ni wajibu wa kila mwanaume na mvulana kusaidia kupatikana kwa usawa kwa wanaume na wanawake katika maeneo yote ambayo yanaonekana kuwa na upendeleo kwa upande mmoja.

“Usawa wa kijinsia sio tu suala la wanawake pekee, ni suala la haki za binadamu ambalo hutuathiri sisi sote. Usawa wa kijinsia sio tu kuwawezesha wanawake, lakini pia huweka huru watu kutoka katika ubaguzi uliowekwa kijamii na majukumu ya kijinsia,” alisema Rodriguez.

Awali Balozi wa Sweden nchini, Katarina Rangnitt alieleza kuwa usawa wa kijinsia unahusisha pia katika kusimamia shughuli mbalimbali ikiwepo za nyumbani kwa wanaume na wanawake kushirikiana kuzifanya kwa pamoja.

Alisema ni muhimu kwa jamii kuelewa kuwa ni jambo lenye maana kuwepo kwa usawa wa kijinsia ili wanawake nao waweze kusaidia shughuli za maendeleo kwa familia na taifa kwa ujumla.

“Usawa uwepo katika sehemu zote hata kazi za nyumbani zifanyike kwa pamoja … ni muhimu kwa mama, baba na kijana kuwepo kwa usawa wa kijinsia kwa watu wote,” alisema Bi. Rangnitt.

Siku ya Wanawake kwa mwaka huu kidunia imekuwa na kauli mbiu ya kimataifa isemayo ‘Dunia 50-50 Ongeza Jitihada kwa ajili ya Usawa wa Kijinsia’ na kitaifa kaulimbiu imekuwa ni ’50-50 ifikapo 2030 Tuongeze Jitihada’.

Balozi wa Sweden nchini, Katarina Rangnitt (wa kwanza kulia), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake nchini, Anna Collins-Falk

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akizindua Kundi la Mshikamano la `HeForShe`.


Mdahalo ukiendelea, (wa kwanza kulia) Katibu Mkuu wa Bazara Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng`i Issa, Kiongozi wa Timu ya Umoja wa Mataifa wa Wanawake ya Uwezeshaji Kiuchumi, Mehjabeen Alarakhia na Mshauri wa Jinsia na Maendeleo, Edward Mhina.

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa hotuba katika mdahalo kuhusu wanawake na uzinduzi wa Kundi la `HeForShe`.

Balozi wa Sweden nchini, Katarina Rangnitt.akitoa hotuba kuhusiana Siku ya Wanawake.

Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake nchini, Anna Collins-Falk

Mshereheshaji wa mdahalo huo, Usu Mallya

Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake nchini, Anna Collins-Falk akikata keki ya kusherekea Siku ya Wanawake Duniani, Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...