Skip to main content

Kilombero Community Charitable Trust wajenga darasa



Mkurugenzi Mtendaji wa Kilombero Sugar Mark Bainbridge akiwaongoza Wazazi na wafanyakazi wa Kilombero Sugar kukagua darasa katika shule ya msingi Muungano lililojengwa kwa ufadhili wa chama cha kusaidia jamii cha Kilombero Community Charitable Trust (KCCT). Hafla hiyo ilifanyika Kilombero mwishoni mwa wiki.



Mkurugenzi mtendaji wa Kilombero Sugar Mark Bainbridge akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi ya Muungano mbele ya darasa la awali lililojengwa kwa ufadhili wa chama cha kusaidia jamii cha Kilombero Community Charitable Trust (KCCT) Hafla hiyo ilifanyika Kilombero mwishoni mwa wiki.


Mwakilishi wa Kilombero Sugar Joseph Rugaimukamu akiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Muungano baada ya kukabidhiwa madawati na chama cha kusaidia jamii cha Kilombero Community Charitable Trust (KCCT), hafla hiyo ya kukabidhi ilifanyika mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro. 


******************


Kiwanda cha Sukari cha Kilombero kimewekeza zaidi ya shilingi milioni 200 katika kipindi cha mwaka jana kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii katika nyanja za afya na elimu, ikiwa ni kurudisha sehemu ya pato lake kwa jamii ambapo kiwanda kinaendesha shughuli zake.

Meneja wa Mfuko wa kusaidia Jamii (Kilombero Community Charitable Trust (KCCT) Mary Elizabeth alisema jana kuwa miradi iliyotekelezwa mwaka jana ni pamoja na ujenzi wa madarasa miwili katika shule za msingi Kalunga na Muungano kwa jumla ya shilingi milioni 38.5.

Alisema kabla ya utekelezaji wa mradi huu, wanafunzi wa chekechea walikuwa wakisomea chini ya mti wa mwembe ambapo masomo yamekuwa yakiahirishwa mara kwa mara kutokana na mvua na wakati mwingine ilibidi kufyeka majani marefu ili kuandaa sehemu ya kusomea.

Mradi mwingine uliotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa vyoo katika shule za msingi Mang’ula and Mgudeni wenye thamani ya shilingi milioni 30. Kila choo kina mashimo sita na sehemu ya kujisaidia haja ndogo na pia kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

“Pamoja na kuwa Mmoja wa wazalishaji wakubwa wa Sukari nchini, pia Kiwanda cha Sukari Kilombero kimekuwa mstari wa mbele kusaidia miradi mbalimbali ya afya na Elimu ili kuweza kuboresha mazingira ya kusomea and afya za Watoto wa wilaya za Kilombero na Kilosa,” alisema.

Aliitaja miradi mingine ya kijamii iliyotekelezwa ikiwa ni Pamoja na ujenzi wa bweni la wasichana katika shulie ya sekondari ya Ruhembe kwa thamani ya shilingi milioni 90 ambalo litaweza kupokea wanafunzi 48. Hii itaondoa usumbufu wa kutembea kwa zaidi ya kilomita 40 kila siku kwa wasichana hawa.

Kwa upande wa afya, Kiwanda cha Sukari Kilombero kinaendelea na ujenzi wa Nyumba ya wafanyakazi wa afya katika hospitali ya Nyandeo wenye thamani ya shilingi milioni 43. Pia katika kuendeleza mashirikiano kati ya Mfuko wa Kusaidia Jamii na Kiwanda cha Sukari wamewekeza zaidi ya shilingi milioni 700.

Akishukuru katika hafla ya makabidhiano, mkuu wa shule ya sekondari ya Ruhembe Bw Johannes Ruekulamu alishukuru Kiwanda cha Sukari Cha Kilombero kwa ujenzi wa bweni ambalo litaongeza ufaulu, nidhamu na kupunguza mimba kwa Watoto wa shule.

Naye mwenyekiti wa kamati ya Wazazi shule ya msingi Muungano Bw Denis Athanas alisema ujenzi wa madarasa utamaliza kabisa tatizo la muda wa zaidi ya miaka sita ambapo wanafunzi wamekuwa wakisomea chini ya mti na mara nyingi wakinyeshewa na mvua au jua kali.






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...