Skip to main content

KLSA ASSOCIATES YAJIUNGA NA PKF, PROF. ASSAD AWATAKA KUONYESHA UBORA ZAIDI




Mgeni rasmi katika halfa ya uzinduzi wa ofisi za PKF Associates, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad akiwasili ukumbini na kukabidhiwa zawadi. (Picha na Rabi Hume wa Modewjiblog)

Katika kuhakikisha wanajitanua katika utoaji wa huduma bora za uhakiki na ukaguzi wa hesabu, kampuni ya KLSA Associates ya nchini imejiunga na mtandao wa kimataifa wa makampuni ya hesabu za kifedha na ushauri ya PKF ambapo baada ya kujiunga imebadilika jina kutoka KLSA Associates na kuwa PKF Associates Tanzania.

Akizungumza katika halfa ya KLSA kujiunga PKF, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad aliwapongeza KLSA kujiunga na PKF na kuwataka kuongeza juhudi na kuboresha huduma zaidi kwa kuzingatia kwa sasa wamejiunga na kampuni ambayo inasifika duniani katika ukaguzi wa hesabu, utunzaji wa hesabu za kifedha, ufumbuzi na ushauri wa masuala ya kodi na kibiashara.

“Tunafahamu jinsi PKF wanavyofanya kazi, mmepata nafasi ya kujiunga nao na itarahisisha kwenu kupata hata taarifa nyingi hivyo ni wakati wa kuonyesha kuwa ninyi ni bora katika kutoa huduma,” alisema Prof. Assad.

Nae Meneja Mshirika wa PKF Associates Tanzania, Mustasir Gulamhussein alisema wameamua kujiunga na PKF kwa kutambua uwezo wao wa kufanya kazi katika maeneo mbalimbali duniani na wanaamini kujiunga kwao kutawawezesha kujitanua katika utoaji wa huduma bora zaidi kutokana na kuwa na wafanyakazi walio na uwezo.

“PKF ni jina linaloheshimika na kutambulika katika uhifadhi wa taarifa za kifedha ulimwenguni na kwa kuwepo Tanzania kunadhihirisha umuhimu wake katika kuwahudumia wateja ambao wanapanua wigo wao kimataifa na tunaamini tutakuwa zaidi katika kutoa huduma,” alisema Gulamhussein.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa PKF Kanda ya Afrika, Theo Veemark alisema KLSA ni kampuni nzuri katika utendaji wao wa kazi za uhakiki na ukaguzi wa hesabu hapa nchini na wanaamini kufanya kazi na KLSA kutawawezesha kutanua huduma zao zaidi na kurahisisha utendaji wa kazi.

“Tunafuraha kuwakaribisha KLSA katika familia ya PKF tunaamini kupitia muungano huu tutaweza kutanua soko letu la kibiashara na kubadilishana mawazo ili tuweze kuboresha huduma zetu zaidi,” alisema Veemark.


Meneja Mshirika wa PKF Associates Tanzania, Mustasir Gulamhussein akielezea KLSA kujiunga PKF na matarajio yao.


Mkurugenzi wa PKF Kanda ya Afrika, Theo Veemark akielezea soko la biashara na jinsi watakavyofanya kazi.



Mkurugenzi Mtendaji wa PKF kwa Afrika Mashariki, Atul Shah akielezea jinsi PKF inavyozidi kujitanua na kupata nafasi ya kuboresha huduma zaidi.


Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad akitoa hutuba na kuwapongeza KLSA kujiunga PKF.



Mshereheshaji wa halfa hiyo, Taji Liundi.


Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad akimkabidhi Meneja Mshirika wa PKF Associates Tanzania, Mustasir Gulamhussein cheti cha PKF kuashiria KLSA kujiunga na PKF.


Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad akikabidhi mfano wa hundi ya Dola 4,000 kwa Shule mbili za Wilaya ya Mkuranga, Pwani kwa ajili ya sola ambazo zitagawiwa kwa wanafunzi.


Mkurugenzi wa PKF Kanda ya Afrika Mashariki, Murtuza Dalal akimkabidhi zawadi ya shukrani Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad.


Meneja Ukaguzi wa PKF Associates Tanzania, Azim Budhwani akitoa neno la shukrani na kufunga halfa hiyo.


Waalikwa wakifurahi baada ya kumalizika kwa halfa hiyo ya KLSA kujiunga na PKF.






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...