Skip to main content

MAANDALIZI YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI TANZANIA 2016/2017 YAANZA RASMI



Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa Akizungumza na wadau wa Utafiti wa Viashiria na matokeo ya Ukimwi wakati wa mkutano wa wadau hao uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa linalojishughulisha na masuala ya Afya – ICAP kutoka chuo cha Colombia New youk, Dkt. Fernando Morales akizungumza mbele ya wadau wa Utafiti wa Viashiria na matokeo ya Ukimwi wakati wa mkutano wa wadau ha oleo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tume ya Kudhiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Bibi. Fatma Mrisho Akizungumza na wadau wa Utafiti wa Viashiria na matokeo ya Ukimwi wakati wa mkutano wa wadau hao uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya wadau. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa wa tatu kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa NBS jijini Dar Es Salaam leo.

Wito umetolewa kwa wadau pamoja na wananchi ili kushiriki kikamilifu katika kuwezesha upatikanaji wa takwimu rasmi nchini.

Akizungumza katika Mkutano wa Wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa amesema wananchi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wana mchango mkubwa katika kufanikisha upatikanaji wa takwimu rasmi nchini.

“Leo hii tumekutana na wadau mbalimbali wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 utakaofanyika mwezi Agosti mwaka huu kwa ajili ya kujadili na kushauriana namna ya kufanya utafiti huu kwa ufanisi ili kupata takwimu bora zitakazosaidia katika kutunga sera na kupanga mipango ya maendeleo nchini”, amesema Dkt. Chuwa.

Dkt. Chuwa amefafanua kuwa utafiti huu unategemea sana ushiriki wa wananchi kwani wao ndio wadau na wahusika wakuu ambao wanapaswa kutoa ushirikiano wa kutosha ili kurahisisha upatikanaji wa takwimu rasmi zitakazosaidia Taifa katika kuboresha huduma za afya kwa manufaa ya watanzania wote.

Dkt. Chuwa amesema Ofisi ya Taifa ya Takwimu ipo katika harakati za kukamilisha maandalizi ya utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania 2016/2017 ambao utaanza kufanyika nchi nzima kuanzia mwezi Juni mwaka huu. 

Aidha Dkt. Chuwa amesema utafiti huu ni wa kipekee ukilinganishwa na tafiti zilizotangulia kutokana na kuongezeka kwa viashiria vitakavyo chunguzwa ikiwemo kuangalia kiwango cha CD4, kiwango cha maambukizi mpya, upatiakanaji wa huduma zinazohusiana na UKIMWI pamoja na kupima watoto wadogo wenye umri chini ya mwaka mmoja.

Amesisitiza kuwa kukamilika kwa utafiti huu kutasaidia Serikali katika kuboresha huduma za afya nchini hasa katika kupambana na maambukizi mapya ya UKIMWI na namna ya kuboresha upatikanaji wa vifaa tiba.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa ICAP nchini, Dkt. Fernando Morales amesema utafiti huu ni wa muhimu katika kupima viashiria na matokeo ya UKIMWI kwa nchi ambazo zimekuwa zikipata msaada wa kupambana na UKIMWI kutoka Serikali ya Marekani.

“Lengo la Utafiti huu ni kupata viashiria ambavyo vinasababisha maambukizi mapya pamoja na kupima jinsi gani Taifa limeweza kupambana na ugonjwa wa UKIMWI nchini”, amesema Dkt. Morales. 


Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 unafanyika katika nchi Ishirini (20) Afrika ambapo kwa sasa nchi nane (8) zinaendelea na utafiti huu zikiwemo Zimbabwe, Zambia, Malawi, , Lesotho, Swaziland, Uganda, Namibia na Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...