Skip to main content

MRADI WA KUKUZA TEKNOLOJIA KUPITIA WATOTO XPRIZE WAZINDULIWA DODOMA



Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Simon Msanjila (kulia) akitoa hotuba ya ufunguzi wa mradi wa kukuza teknolojia kupitia watoto XPRIZE uliofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mwandamizi wa Uendeshaji kutoka Taasisi ya XPRIZE, Matt Keller, Kaimu Mkurugezi wa Elimu ya Msingi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Kassim Kaoneka na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodrigues. (Picha na Modewjiblog)

Kwa kutambua uwezo walionao watoto katika kubuni vitu mbalimbali, Taasisi ya XPRIZE iliyo na makazi yake nchini Marekani, imezindua mradi wa XPRIZE nchini ambao utahusisha watoto ambao hawapo shuleni ukiwa na malengo ya kukuza teknolojia ya dunia kwa kutumia uwezo walionao watoto wa miaka 5-12.

Akielezea mradi huo, Mkurugenzi Mwandamizi wa Uendeshaji kutoka Taasisi ya XPRIZE, Matt Keller, alisema kuwa wameanzisha mradi huo kwa kutambua uwezo ambao wanao watoto na kama wakiwezeshwa wanauwezo wa kufanya mambo makubwa.

Alisema dunia ina watoto wengi ambao hawapo shuleni kwa sababu mbalimbali na hivyo mradi huo utakwenda kufanyika kupitia watoto ambao hawapo mashuleni na watawapatia vifaa mbalimbali ili waweze kupimwa uwezo wao katika kazi zinazohusiana na teknolojia.

“Dunia ina watoto Milioni 57 ambao hawapo shuleni tutawatumia kama hao kwa sababu tunaamini watoto wanaweza kufanya mambo mengi lakini wanachohitaji ni kuwezeshwa ili waweze kukamilisha mambo wanayofanya,” alisema Keller.

Nae Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues alisema kuwa ni muda muafaka kwa watoto kusaidiwa kupata elimu kwa njia ya kiteknolojia hasa kwa wakati uliopo ambao teknolojia inatumika zaidi katika kurahisisha kazi mbalimbali.

Alisema ni muhimu kwa Tanzania kuanza kutumia mifumo ya teknolojia hasa katika kipindi hiki ambacho nchi ipo katika hatua za kuelekea uchumi wa kati kwani kwa kufanya hivyo itaweza kurahisha kufikiwa malengo kwa muda muafaka ambao umepangwa.

“Ni wakati kwa watoto kupata elimu ya teknolojia, haijalishi hayupo shuleni kwa kipindi hiki teknolojia inatumika zaidi na hii itasaidia wakati huu ambao nchi (Tanzania) inakwenda katika uchumi wa kati,” alisema Bi. Rodrigues.


Nae Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Simon Msanjila alisema kuwa serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ili kuwawezesha watoto kupata elimu ya teknolojia lakini inakuwa ni ngumu kufikia malengo hayo yenyewe hivyo ni tumaini lao mradi huo utafanikiwa.

Alisema ni muhimu kwa watoto kupatiwa elimu ya teknolojia kwa dunia ya sasa na serikali ipo tayari kushirikiana nao kwa pamoja ili mradi huo uweze kufanyika kama jinsi umevyopangwa na Taasisi ya XPRIZE ambao ndiyo waanzilishi wa mradi huo ambao unataraji pia kufanyika nchi mbalimbali duniani.

“Unaposema dunia inakuwa kijiji ina maana unazungumza kuhusu teknolojia kutokana na kusogeza kila jambo karibu na kwa haraka ni ngumu kwa serikali kufanya yenyewe lakini wanapopattikana watu wanaosaidia inakuwa vizuri na pia inasaidia kukuza teknolojia nchini,” alisema Prof. Msanjila.

Nae Afisa Mradi wa Elimu wa UNESCO, Faith Shayo alisema mradi huo nchini utaanza kwa majaribio katika makundi 200 kutoka mkoa wa Tanga katika wilaya ya Lushoro, Korogwe, Muheza, Pangani, Mkinga, Handeni na Kilindi na mkoa wa Arusha utafanyika katika wilaya ya Ngorongoro ambapo watoto hao watapatiwa simu zilizo na muundo wa tablet na sola za kuchajia na watatumia 'tablet' kwa kusoma, kuandika na kuhesabu na baada ya hapo watakuwa wakichaguliwa kutokana na uwezo binafsi.


Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa XPRIZE uliofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Kaimu Mkurugezi wa Elimu ya Msingi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Kassim Kaoneka. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Simon Msanjila.


Naibu wa Programu kutoka Shirika la Chakula Duniani (WFP) nchini, Marina Negroponte (kulia) akizungumzia nafasi ya Shirika lake katika utekelezaji wa mradi wa XPRIZE katika hafla fupi ya uzinduzi wa mradi huo iliyofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.


Pichani juu na chini ni Mkurugenzi Mwandamizi wa Mafunzo kutoka Taasisi ya XPRIZE, Matt Keller akizungumzia malengo ya mradi huo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.






Makamu wa Rais anayeshughulikia uendeshaji wa XPRIZE Foundation, Joel Carnes akifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye uzinduzi wa mradi huo uliofanyika mjini Dodoma, mwishoni mwa wiki.


Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Simon S. Msanjila (kushoto) akijadili jambo na Mkurugenzi wa Elimu ya Msingi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Sarah Mlaki wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa kukuza teknolojia kupitia watoto XPRIZE uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.


Kutoka kulia ni Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues, Kaimu Mkurugezi wa Elimu ya Msingi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Kassim Kaoneka, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Simon Msanjila wakifuatilia kwa umakini 'power point presentation' ya jinsi mradi huo utakavyotekelezeka nchini.


Afisa Mradi wa Elimu wa UNESCO, Faith Shayo akizungumzia utekelezaji wa mradi huo wa kukuza teknolojia kupitia watoto XPRIZE na wadau watakaoshirikiana nao katika kutekeleza.


Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugezi wa Elimu ya Msingi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Kassim Kaoneka, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Simon Msanjila, Mkurugenzi wa Elimu ya Msingi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Sarah Mlaki, waandishi wa habari pamoja na wadau wa sekta elimu waliohudhuria uzinduzi huo, mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.


Naibu wa Programu wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) nchini, Marina Negroponte akiandika mambo muhimu kwenye uzinduzi wa mradi wa XPRIZE.


Afisa mradi wa Elimu wa Unesco, Dar es Salaam, Faith Shayo akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mwandamizi wa Uendeshaji kutoka Taasisi ya XPRIZE, Matt Keller wakati wa uzinduzi wa mradi wa XPRIZE uliofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.


Baadhi ya wadau wa sekta ya elimu, waandishi wa habari na viongozi kutoka Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi waliohudhuria uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Hoteli ya Veta, mjini Dodoma.


Baadhi ya wageni waalikwa wakibadilishana mawazo kwenye uzinduzi wa mradi wa XPRIZE uliofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.


Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Simon Msanjila akiagana na Mkurugenzi Mwandamizi wa Uendeshaji kutoka Taasisi ya XPRIZE, Matt Keller....Kulia Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues na kushoto ni Makamu wa Rais anayeshughulikia uendeshaji wa XPRIZE Foundation, Joel Carnes.


Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Simon Msanjila akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa mikutano wa Veta mara baada ya kuzindua rasmi mradi huo.


Mkurugenzi Mwandamizi wa Uendeshaji kutoka Taasisi ya XPRIZE, Matt Keller (katikati) akizungumza na mmoja wa waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Veta mjini Dodoma, mara baada ya uzinduzi wa mradi huo. Kulia ni Makamu wa Rais anayeshughulikia uendeshaji wa XPRIZE Foundation, Joel Carnes.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...