Skip to main content

TRA YAWAANDALIA ZAWADI NONO WAANDISHI WA HABARI WALIOSHINDA TUZO YA UANDISHI WA KODI NA MAKUSANYO YA MAPATO


Pichani ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Richard Kayombo, kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA (Kushoto) akimkabidhi tuzo pamoja na cheti mshindi wa kwanza wa tuzo ya Uandishi wa habari za Kodi na Makusanyo ya Mapato ya Serikali kwa mwaka 2015 Bi. Valeria Mwalongo katika sherehe za kutunuku waandishi bora wa mwaka zilizofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam tarehe 29 Aprili 2016

Mshindi wa pili wa tuzo ya Uandishi wa habari za Kodi na Makusanyo ya Mapato ya Serikali mwaka 2015 Bw. Nuru Hassan (kulia) akipokea cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Richard Kayombo (kushoto) aliyemuwakilisha Kamishna Mkuu wa TRA katika sherehe zilizofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam tarehe 29 Aprili 2016


Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tuzo za Umahiri katika Uandishi wa Habari, ambazo hutolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT), waandishi wawili wameshinda tuzo ya Uandishi wa Kodi na Makusanyo ya Mapato ya Serikali kwa mwaka 2015,


Waandishi hao wawili, Valeria Mwalongo, mwandishi wa Redio Tumaini aliyeshika nafasi ya kwanza na Bw. Nuru Hassan kutoka Afya Redio aliyeshika nafasi ya pili katika kinyang’anyiro hicho ni washiriki na washindi wa kwanza kupata tuzo hiyo ambayo imeingizwa kwa mara ya kwanza kwa kazi za mwaka 2015.


Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka TRA Bw. Richard Kayombo alitoa tuzo hiyo kwa waandishi hao kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA katika Ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam ambako sherehe za kutunuku Zawadi zilifanyika.


Kutokana na ushindi huo Bw. Richard Kayombo amesema TRA itatoa donge nono kwa waandishi wa habari watakaoshiriki na kushinda katika kundi la uandishi wa habari za kodi na ukusanyaji wa mapato. Mshindi wa kwanza wa 2015 Bi. Valeria Mwalongo atajipatia kompyuta mpakato na wapili Bw. Nuru Hassan atajipatia simu aina ya Samsung mbali na kupata tuzo na vyeti kutoka MCT.


“Mamlaka ya Mapato Tanzania imedhamiria kuwajengea uwezo zaidi wanahabari kwa kuwaelimisha juu ya masuala ya kodi kwa kushirikiana na MCT ambao waowatawajengea uwezo juu ya uandishi bora kwaajili ya kuchochea ushindani zaidi katika kundi hili mwaka ujao kwa kazi ambazo zitaandikwa katika mwaka huu wa 2016.” Alisema Bw. Kayombo


MCT ilianzisha kundi la tuzo za uandishi wa habari za kodi na ukusanyaji mapato baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania kuomba kundi hili liingizwe katika tuzo hizo kwa kuzingatia kwamba waandishi na watangazaji wa habari wanaweza kushiriki kwa kuandika masuala ambayo yataongeza ridhaa ya kulipa kodi kwa hiari.


Sehemu ya barua ya TRA kwa MCT inasema, “TRA inatekeleza majukumu mbalimbali na mojawapo ni kuihabarisha jamii kupitia vyombo mbalimbali. TRA pekee haiwezi kufanikisha jukumu hili bila kuwashirikisha wadau ndio maana inaiomba MCT kuanzisha kundi la tuzo ya uandishi wa masuala ya kodi”


Tuzo ya kundi la uandishi wa Kodi na ukusanyaji mapato ya serikali ilijumuisha habari mbalimbali za masuala ya kodi, masuala ya ukusanyaji wa kodi, umuhimu na matumizi ya kodi hasa katika kugharimia huduma za jamii, nidhamu ya ukusanyaji na utumiaji, mianya ya upotevu wa mapato, njia za kuongeza wigo wa kodi. Nia ni kuongeza uhiari wa ulipaji kodi kwa ili kukuza mapato ya serikali


MCT ilizindua uwasilishaji wa kazi za wanahabari tarehe 12 Februari 2016 kwa makundi 22 yaliyojumuisha uandishi wa habari za Uchumi na Biashara, Michezo na Utamaduni, Mazingira, Watoto, Virusi vya Ukimwi na Ukimwi, Utawala Bora, Jinsia, Sayansi na Teknolojia, Afya ya Uzazi, Uandishi wa Uchunguzi, Elimu, Utalii na Uhifadhi, walemavu, Mpiga picha bora wa magazeti, Mpiga picha bora, Mchoraji kibonzo bora, Afya ya Uzazi kwa Vijana, Gesi, petrol, Utafiti wa Madini pamoja na habari za kodi na ukusanyaji mapato.


TRA inatoa wito kwa waandishi wote kujitokeza kwa wingi zaidi kuwania kinyang’anyiro hiki katika mashindano ya mwaka ujao ili kuendelea kupaza sauti juu ya masuala mbalimbali yahusuyo kodi na kujishindia zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa kipindi hicho.
“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...