Skip to main content

HIFADHI YA TAIFA YA RUAHA KINARA KWA UJANGILI WA TEMBO NCHINI

Mwalimu wa Uchumi na Utalii Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),  Profesa Wineaster Anderson (kulia), akitoa mada kuhusu uchumi na Utalii katika mkutano wa mwaka wa Hifadhi za Taifa Tanzania na wanahabari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali mjini Morogoro leo.
Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA), Ibrahim Mussa (kulia), akitoa mada katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI), Dk. Felician Kilahama (kulia), akitoa mada kuhusu misitu katika mkutano huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA), Dk.Allan Kijazi, akizungumza jana katika mkutano huo.
Wanahabari Khadija Khalili (kushoto) na Beatrice wakiwa kwenye mkutano huo.
Wahariri, Bakari Kimwaga (kushoto) na Anicetus Mwesa wakifuatilia mkutano huo.


Mwanahabari Lazaro kulia akijiandikisha katika kitabu cha mahudhurio
Wanahabari na wahariri wakiwa kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama cha wamiliki wa Blogu Tanzania (TBN), Joachim Mushi akiwa kazini katika mkutano huo ulihudhuriwa na baadhi ya bloger.
Mhariri wa Nipashe, Jesey Kwayu akiuliza maswali.
Mwanahabari na mpiga picha wa gazeti la mtanzania, Humphrey Shao akiuliza maswali.
'Hapa ni kazi tu' wanahabari wakichukua taarifa mbalimbali za mkutano huo.

Na Dotto Mwaibale

MKURUGENZI Mkuu wa Hifadhi za Taifa (Tanapa), Dk. Allain Kijazi amesema Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ni kinara wa ujangili wa Tembo ukilinganisha na hifanyi nyingine

Dk. Kijazi ameyasema hayo leo mkoani Morogoro katika siku ya pili ya Mkutano wa Mwaka wa Hifadhi za Taifa Tanzania ulioandaliwa kwa kwa ajili ya wahariri na wanahabari waandamizi wa vyombo mbalimbali vya habari.

"Hali hii ya  ujangili inatokana na kuwepo kwa tembo wengi ambapo majangili wamekuwa wakiingia katika hifadhi hiyo na kufanya uharifu" alisema Kijazi.

Aliongeza kuwa kutokana na hali hiyo jitihada kubwa zinafanya kwa kutumia mfumo wa kiokorojia kwa lengo la kuhakikisha udhibiti wa ujangili unafanikiwa na kunusuru ujangili huo unaotishia katika hifanyi hiyo.


Katika hatua nyingine Dk.Kijazi ametoa mwito kwa Serikali kutengeneza miundo mbinu ya barabara na Wawekezaji kujenga mahoteli katika mikoa ya Kusini na Magharibi mwa Tanzania ili kukuza utalii katika maeneo hayo jambo litakalo inua uchumi wa maeneo hayo na Taifa kwa ujumla.

Aliongeza kuwa baadhi ya mikoa ya Kusini na Magharibi mbayo inavivutio vya utalii lakini imeshindwa kufanya vizuri katika kuingiza watalii wengi kutokana na miondo mbinu yake ya barabara kutokuwa rafiki.

"Ninaamini waandishi wa habari mkitupigia debe na Serikali ikasikilia kilio hiki na kutengeneza barabara kwa kiwango kizuri na Wawekezaji wakajenga mahoteli hakika itasaidia kuvutia watalii kama ilivyo kwa mikoa ya Kaskazini," alisema.

Alifafanua kuwa mikoa ya Kaskazini ambayo inavivutio imekuwa ikipata watalii wengi kutokana na urahisi wake kufikika kwa maana watalii wanahitaji kutumia muda mfupi kufika mbugani ili atumie muda mrefu kuona wanyama.

Aliongeza kuwa hali hiyo ni tofauti na mikoa ya Kusini na Magharibi ambako mtalii atatumia murefu barabarani na kutumia muda mfupi katika kuangalia wanyama na vivutio vingine jambo ambalo si lengo lake.

Alisema licha miundo mbinu ya barabara za Kusini kutokuwa rafiki kufika katika vivutio, pia hata malazi kwa watalii si ya kuvutia na pengine hakuna kabisa hivyo ni changamoto kwa wawekezaji kuhakikisha wanajenga mahoteli ya kisasa.

Aliweka wazi kuwa ikiwa jambo hilo litafanikiwa kwa kuwa na miundombinu mizuri ya barabara na hoteli zenye viwango hakika watalii katika mikoa ya Kusini wataongezeka.


Wakati huo huo, Mkurugenzi wa Masoko Tanapa, Ibrahimu Mussa alisema kuwa ili kuinua mapato yanayotokana na utalii nchini malipo ya watalii yanafanyika kwa kadi za kibenki.

"Tumeamua kuondokana na upokeaji wa fedha kwa 'Cash' ili kuondoa upotevu wa mapato jambo litakalosaidia kuinua kiwango cha ukusanyaji wa mapato tofauti na ilivyokuwa awali,"alisema.

Akizungumzia suala baadhi ya watalii kulipia gharama viingilio wakiwa nchini kwao, alisema fedha wanazolipa zinafika Tanzania na lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha watalii wanakuwa salama katika mali zao.

Aliongeza kuwa hata mtalii akiumia akiwa hapa nchini akiwa kwenye utalii analipwa bima kupitia nchi yake jambo ambalo linamfanya kuwa salama zaidi.

Pia alisema Tanzania imeshuka katika viwango vya vivutio vya asili ikitoka namba mbili nyuma ya Brazil hadi na namba saba na katika viwango vya jumla inashika nafasi ya 93 kati ya nchi 114 zenye ushindani.

Alifafanua kuwa sababu ya kushuka katika viwango hivyo vya dunia ni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uvamizi wa maeneo ya vivutio hivyo na miundo mbinu ya barabara na changamoto zingine zilizopo.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...