Skip to main content

MKOA WA IRINGA UNA WATUMISHI HEWA 169

Mkoa wa Iringa iliunda timu ya wataalam kwa ajili ya kupita katika Hospitali Teule zote za Wilaya na kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa lengo la kuendelea kubaini iwapo wapo watumishi hewa ambao hawakubainishwa katika zoezi la awali. 

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema kuwa timu niliyounda imekamilisha kazi yake tarehe 07/06/2016 na kunikabidhi taarifa yake. Kwa ufupi taarifa hiyo imebainisha masuala mbalimbali.

Akiongea na waandishi wa habari jana alisema kuna watumishi hewa 169 katika Halmashauri ambao wamekuwa wakipokea mishahara pasipo kustahili kutokana na utoro, kustaafu na kufariki. 

Aidha, alisema kuwa upotevu wa fedha kutokana na ulipaji wa mishahara isivyostahili umeisababishia Serikali hasara ya shilingi Milioni 364,028,910.80. 

Timu hiyo pia imebaini kuwa, katika Hospitali Teule ya Ilula inayotoa huduma katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo lipo tatizo la fedha za mishahara isiyolipwa inayofikia kiasi cha Shilingi Milioni 151,583,969.00 kutorejeshwa Hazina tangu Januari, 2008 hadi Februari, 2016. 

Fedha hiyo imetumika kwa shughuli za uendeshaji wa Hosipitali Teule ya Wilaya ya Ilula pasipo idhini ya Serikali. Fedha hiyo ilitumika kugharamia huduma za umeme, ununuzi wa dawa na kulipa mishahara ya watumishi ambao orodha yake haikuwa inafahamika na Serikali kunyume na taratibu. 

Mkoa unaendelea kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa katika taarifa ya Tume na ninaahidi kuendelea kutoa taarifa ya utekelezaji baada ya kuyafanyia kazi.

UTEKELEZAJI WA UPATIKANAJI WA MADAWATI

Mkoa una jumla ya shule za Msingi 478 na shule za Sekondari 107 zinazo milikiwa na Serikali. 

Awali Mkoa ulikuwa na upungufu wa Madawati 29,347, ikiwa Madawati 26,046 ni upungufu katika shule za Msingi, na Madawti 3,301 ni upungufu katika shule za Sekondari.

Hadi kufikia tarehe 06/06/2016, Halmashauri zimetengeneza jumla ya Madawati 17,225 kwa ajiri ya shule za Msingi na Sekondari. Hivyo kubaki na upungufu wa Madawati 4,681.

Hadi kufikia tarehe 6/6/2016 Mkoa umetengeneza jumla ya Madawati 442 na bado jitihada zinafanyika kwa ajili ya kuongeza zaidi idadi hiyo. 

HALI YA UPATIKANAJI WA SUKARI KATIKA MKOA WA IRINGA

Mkoa wa Iringa hauna kiwanda cha uzalishaji wa sukari. Kutokana na kukosekana kwa uzalishaji wa sukari kwa Mkoa wetu tunategemea sukari inayozalishwa kutoka mikoa mingine. Sukari hiyo huletwa Mkoani hapa na Mawakala walioteuliwa na Bodi ya sukari. Mahitaji ya sukari kwa Mkoa wa Iringa kwa mwaka ni tani 14,000, kati ya tani hizo, Walaji wa kawaida hutumia tani 9,000 na matumizi ya viwanda ni tani 5,000.

Hali ya upatikanaji wa sukari

Changamoto ya upungufu wa sukari hapa Mkoani imeanza mwezi Machi, 2016 hadi sasa. Kabla ya huu mwezi changamoto haikuwepo na sukari ilikuwa inauzwa kwa bei ya jumla Tsh.88,000 kwa kg. 50 na bei ya reja reja ilikuwa inauzwa Tsh.1,800-2,000 kwa Manispaa ya Iringa na Tsh.2,000-2,200 kwa Halmashauri za Wilaya hususan maeneo ya Vijijini. 

Kwa sasa inauzwa kwa bei ya jumla Tsh.110,000 kwa kg. 50 na bei ya rejareja inauzwa kati ya Tsh. 2,800 na Tshs. 3,000 kwa Manispaa ya Iringa, na Tsh.3,000-3,400 kwa Halmashauri za Wilaya na maeneo ya Vijijini. 

Hatua zilizochukuliwa kukabiliana na upungufu wa Sukari Kuhamasisha Mawakala wa sukari kuleta sukari nyingi.

Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kubaini wanaouza bei ya juu na kuchukua hatua stahiki.

"Nichukue nafasi hii kuwatoa hofu wananchi wa Mkoa wa Iringa na hasa waumini wa dini ya Kiislamu ambao wameanza mfungo mtukufu wa Ramadhani kuwa, katika kipindi chote cha Mfungo Mtukufu na baada ya mfungo kuwa sukari itaendelea kupatikana," alisema Masenza. 

Mawakala wataendelea kuleta Sukari ya kutosha kukidhi mahitaji ya wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...