Skip to main content

MKOA WA IRINGA WAMALIZA TATIZO LA UPUNGUFU WA MADAWATI





MKOA wa Iringa umetekeleza agizo la Rais Dk John Magufuli kwa kufanikiwa kumaliza tatizo la upungufu wa madawati 29, 347 ambayo kati yake 26,046 ulikuwa ukizikabili shule za msingi 478 na 3,301 uliokuwa ukizikabili shule 107 za sekondari.


Akikabidhi sehemu ya madawati hayo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye karakana ya chuo cha Ufundi Stadi (VETA) mjini Iringa jana, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema mpaka jana madawati 21,304 yalikuwa yamekamilika na kusambazwa katika shule hizo.


“Hadi leo tuna madawati 21,304 yaliyokamilika huku madawati 8,163 kwa ajili ya shule za msingi na 1,264 kwa ajili ya shule za sekondari yakiendelea kutengenezwa katika karakana mbali mbali na fedha kwa ajili ya matengenezo hayo tayari zimelipwa,” alisema.


Alisema madawati yaliyochelewa kukamilika ndani ya muda uliopangwa yatakuwa yamekamilika ifikapo Julai 15, mwaka huu na yatasambazwa kwa shule hizo haraka iwezekanavyo.


“Yamechelewa kukamalika kwasababu mafundi waliopewa kuifanya kazi hiyo, walielemewa na kazi yenyewe iliyohitaji uharaka na umakini kwa pamoja,” alisema.


Alisema kazi ya kutengeneza madawati hayo imefanywa kupitia bajeti za halmashauri husika na michango ya wadau mbalimbali wa maendeleo wa mkoa wa Iringa walioko nje na ndani ya halmashauri husika.


“Nishukuru zoezi lililoagizwa na mheshimiwa rais limetekelezwa kutokana na mwitikio mzuri tulioupata kutoka kwa wadau wetu wa maendeleo,” alisema..


Alisema Rais Magufuli alitoa agizo kwa wakuu wote wa mikoa nchini kuhakikisha wanafunzi wote wanakaa katika madawati ifikapo Juni 30 mwaka huu.


Kwa kuzingatia agizo hilo, Masenza alisema alilazimika kuwashirikisha wakuu wake wa wilaya ambao kwa kushirikiana na wadau hao wamesaidia kumaliza upungufu huo.


Akizungumzia mchango wa mkoa katika kufanikisha agizo hilo la Rais, Masenza alisema kwa msaada wa wadau mbalimbali ofisi yake ilitengeneza madawati 700.



Masenza alisema kati ya madawati hayo, 200 ameyatoa kwa halmashauri ya manispaa ya Iringa, Mafinga Mji madawati 100, Iringa Vijijini madawati 100, Mufindi madawati 100 na Kilolo madawati 100.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...