Skip to main content

RIPOTI YA UNHCR YAONESHA UWAPO WA WAKIMBIZI MARADUFU KATIKA HISTORIA YA BINADAMU




TAARIFA ya hali ya wakimbizi duniani kufikia mwaka 2015 inaonesha kwamba watu milioni 65.3 wanaishi kikimbizi ikilinganishwa na watu milioni 59.5 kwa mwaka 2014.

Ongezeko hilo la watu milioni 5.8 katika kipindi cha miezi kumi na mbili kimelezwa kuwa ni la kiwango cha juu tangu kuanzishwakwa Umoja wa Mataifa.

Katika taarifa yake kuadhimisha siku ya wakimbizi duniani (Global Trends) Shirika la Kuhudumia wakimbizi (UNHCR) limesema dunia kwa sasa inakabiliwa na kundi kubwa la watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao kwa sababu mbalimbali ikiwamo migogoro ya kivita, ubaguzi na uvunjaji wa haki za binadamu.

“Takwimu zilizopo leo hii, aina ya migogoro iliyopo na ugumu wake kumesababisha kuwapo na wimbi kubwa la wakimbizi tangu kuanzishwa tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa; watu milioni 60 wameondolewa katika makazi yao duniani hapa. Kila siku janga la wakimbizi linatangazwa katika vyombo vya habari ; watoto, wanawake na wanaume wakipoteza maisha yao katika jaribio la kukimbia vurugu zilizopo katika eneo lao" anasema Filippo Grandi, Mkuu wa UNHCR.

Kati ya wakimbizi milioni 65.3, wakimbizi milioni 3.2 wako katika nchi zenye viwanda wakisubiri kutambuliwa hadhi zao kama wakimbizi, milioni 21.3 wametawanyika duniani kote na milioni 40.8 wamelazimika kukimbia maeneo yao lakini wapo katika nchi zao.




Mwakilishi wa UNHCR Tanzania, Bi Chansa Kapaya akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya wakimbizi duniani yaliyofanyika katika kambi ya wakimbizi, wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.


Imeelezwa kuwa kwa kuzingatia idadi ya watu waliopo duniani takribani bilioni 7.349 ina maana kwamba mtu mmoja kati ya watu 113 ama anatafuta hifadhi, amekimbia makazi yake lakini yupo katika nchi hiyo hiyo au ni mkimbizi.

Kimsingi duniani kwa sasa kuna watu wengi waliolazimishwa kuhama makazi ya kuliko idadi ya watu waliopo Uingereza, Ufaransa au Italia.

Miaka 10 iliyopita, mwishoni mwa mwaka 2005, UNHCR ilirekodi wastani wa watu sita kukosa makazi kila dakika duniani lakini sasa ni wa 24 kila dakika.

Watu milioni 1.8 walilazimika kukimbia nchi zao kwa mwaka 2015 ukilinganisha na watu milioni 2.9 mwaka 2014.

Uturuki iliorodhesha idadi kubwa ya wakimbizi wapya wakiwamo 946,800 kutoka Syria. Urusi walikuwa na wakimbizi 149,600 kutoka Ukraine. Na vurugu zilipoibuka Burundi mwezi Aprili, karibu watu 123,400 walikimbilia Tanzania.



Kwa idadi hiyo Tanzania inakuwa nchi ya tatu kwa kuhifadhi wakimbizi wengi duniani.


Wakati wakimbizi wapya wa Burundi wanaingia Tanzania,UNHCR ilikuwa katika operesheni ya kuwawezesha wakimbizi waliopo kuendelea na maisha yao ya kawaida. Aidha katika kipindi hiki Tanzania ilitoa uraia kwa wakimbizi wa Burundi walioingia nchini mwaka 1972 ambao walikuwa wakiishi Tabora na Katavi na Marekani iliwapokea wakimbizi 30,000 wa Kongo waliokuwa wakiishi Nyarugusu, Kigoma.

Tangu kuanza kwa wimbi jipya la wakimbizi kutoka Burundi zaidi ya watu 141,000 wamekimbilia Tanzania kutafuta hifadhi na kuifanya Tanzania kuwa nchi inayohifadhi wakimbizi wengi kutoka Burundi.

Asilimia 77.9 ya wakimbizi hao wapya ni wanawake na watoto, Watoto wengi waliofika Tanzania ni wale waliozaliwa katika ardhi ya Tanzania (63,961) wamehifadhiwa katika kambi ya Nyarugusu, moja ya kambi kubwa duniani ikiwa na wakimbizi 131,733.Mazingira ya maisha yao yakiwa magumu. Moja ya vitu ambavyo vinafanywa na UNHCR ni kuwatawanya wakimbizi hao ili kuleta nafuu katika kambi hiyo.

Wakimbizi wengine wapo katika kambi za Nduta na Mtendeli zilizofunguliwa Oktoba 2015 na Januari 2016 kwa lengo la kupunguza msongamano katika kambi ya Nyarugusu na wakati huo huo kutoa nafasi kwa wakimbizi wapya.

Hata hivyo Nduta haraka sana ilifikia kiwango chake cha juu kinachopaswa kuwepo hapo Ilipofika Aprili mwaka huu; Kambi hiyo ina wakimbizi 55,000. Wakimbizi wapya kwa sasa wanapokelewa kambi ya Mtendeli ambapo wakazi wake waliongezeka kufikia 21,796.


Lipo eneo jingine linafikiriwa kufanywa kambi ya wakimbizi eneo la Karago, lakini eneo hili lina matatizo ya maji na haifikiriwi kwamba inaweza kubeba wakimbizi 50,000 wanaotarajiwa kuingia Tanzania kutoka Burundi.

“Wahisani wa kimataifa wameweza kuitikia wito wa kukabiliana na wimbi la wakimbizi wa Burundi na hivyo kuipunguzia mzigo serikali ya Tanzania,UNHCR na Mashirika mengine ya Umoja wa pamoja na taasisi zisizo za kiserikali. hata hivyo bado kunatakiwa raslimali nyingi zaidi ili kukabilina na wimbi hilo,” anasema Mwakilishi wa UNHCR Tanzania, Bi Chansa Kapaya.

UNHCR Tanzania imepata asilimia 40 ya mahitaji yake kusaidia wakimbizi wa Burundi mwaka kukiwa na pengo la dola za Marekani milioni 44.8 hadi kufikia Juni 19,2016.Kwa mantiki hiyo fedha kwa ajili ya kusaidia wakimbizi wa Burundi wanaotarajiwa kufikia 330,000 mwishoni mwa mwaka huu zipo kidogo sana.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...