Skip to main content

ZITTO KABWE AJILIPUA TENA BUNGENI,AWALIZA WABUNGE



ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo amekoleza moto wa wabunge kukatwa kodi katika fedha za kiinua mgogo, anaandika Dany Tibason.


Wakati hayo yakifanyika, Serikali ya Rais John Magufuli imewang’oa wabunge wa viti maalumu kushiriki kwenye Kamati za Fedha na Mipango za Halmashauri.


Jumatano wiki hii serikali ilisoma bajeti yake ya Sh. 29. 52 kwa Mwaka wa Fedha 2016/17, sehemu ya bajeti hiyo ilionekana kukera wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).


“Mheshimiwa spika, natangaza kufuta msamaha wa kodi ya mapato kwenye malipo ya kiinua mgongo kinacholipwa kwa wabunge kila mwisho wa muhula wa miaka mitano ili kujenga misingi ya usawa na haki katika utoaji wa kodi kwa kila mtu anayestahili kulipa kodi,” alisema Dk. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango.


Kutokana na mpango huo wa serikali kutoza kodi katika kiinua mgongo cha wabunge na kuzua zogo kwa wabunge wa CCM, Zitto amesema, ni vema serikali ikafanya hivyo ili kuongeza wigo wa ukusanyaji kodi kwa ajili ya kuendesha nchi.


Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini amekwenda mbali zaidi na kusema kwamba, Bunge halipaswi kuishia kwenye kodi hiyo pekee kwa kuwa, kuna kodi nyingi za wabunge ambazo hazijaguswa.


Kauli hio ni mwendelezo wa msimamo wake wa kupinga wabunge kulipwa posho za vikao vya bunge. Katika kampeni yake kwenye Bunge la 10, Zitto hakufanikiwa kuondoa posho hiyo.


Zitto ametoa msimamo wake kuhusu kukata kodi wabunge wakati akitoa maoni yake kwenye uchambuzi wa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/17 ulioandaliwa na Kampuni ya Ukaguzi wa Hesabu za KPMG juzi.


Hata hivyo Zitto amesema kwamba, pamoja na serikali kuanzisha kiinua mgongo hicho lakini hakuna sheria yoyote inayoruhusu kitu hicho kufanyika na hivyo kuonesha kushangazwa na hatua hiyo.


Hatua ya Zitto bila shaka itakoleza mjadala wa posho ambao tayari CCM wameonesha kukerwa na hatua ya serikali kuanza kutoza kodi hiyo.
Wakati Waziri Mpango akiwasilisha bajeti hiyo na kufikia kipengele kinachoelekeza kuwa, kodi hiyo itaanza kukatwa, wabunge wa CCM ambao ndio pekee waliokuwa bungeni, walianza kuguna hatua mbayo ilimlazimu Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika wa Bunge kuingilia kati na kutuwatuliza.
Wakati hayo yakiendelea, serikali imeendelea kuwakomba posho wabunge baada ya Seleman Jafo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kueleza kuwa, wabunge wa viti maalum ni marufuku kushiriki kwenye Kamati za Fedha na Mipango za Halmashauri.
Jafo amesema, kwa mujibu wa sheria za Mamlaka za Wilaya na Mamlaka za Miji, wabunge hao hawaruhusu kushiriki kwenye kamati hizo.
Na kwamba, ili wabunge hao waweze kushiriki kwenye kamati hizo, inahitajika kubadili sheria kwanza ili pendekezo hilo liweze kutekelezeka.
Jafo ametoa kauli hiyo jana wakati akijibu swali la Martha Umbula, Mbunge wa Viti Maalum (CCM) na kwamba, Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Halmashauri wametajwa katika kifungu cha 75(6) cha sheria sura 287 Mamlaka za Wilaya na
kifungu cha 47(4) cha Sheria Sura 288 Mamlaka za Miji.
“Kwa mujibu wa sheria hizo mbili wajumbe wa Kamati hawatazidi theluthi ya Madiwani wote isipokuwa Kamati ya Fedha na Mipango ambayo wajumbe wake ni wale wanaoingia kwa nyadhifa zao,” amesema Jafo.
Amesema, upatikanaji wa wajumbe wa kamati hiyo umefafanuliwa katika Kanuni za Kudumu za Uendeshaji wa kila Halmashauri.
Ameaja wajumbe wake kuwa ni Mwenyekiti au Meya wa Halmashauri, Makamu au Naibu Meya, Mbunge au wabunge wa majimbo, wenyeviti wa kamati za kudumu na wajumbe wasiozidi wawili.
Amesema, wajumbe wa Kamati ya Fedha wataendelea kuwa hao waliotajwa katika Sheria na Kanuni za Mamlaka za Serikali za Mitaa hadi hapo
sheria itakapofanyiwa marekebisho kwa kushirikiana na wadau mbalimbali

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...