Skip to main content

TECNO WAZINDUA SIMU KALI YA CAMON C9


MENEJA MAUZO KUTOKA KAMPUNI YA TECNO MOBILE FRED KADELANE AKIONYESHA SIMU HIYO MARA TU BAADA YA KUZINDUA. WATEJA MIA MOJA WA KWANZA WALIFANIKIWA KUPATA SIMU ZAO.
Tecno Mobile imezindua simu mpya aina ya CAMON C9 yenye uwezo wa hali ya juu katika kupiga picha, uwezo wa 4G LTE na teknolojia mbali mbali za kisasa


Tecno Camon C9 iliyoanza kuuzwa toka tarehe 25 Juni 2016. Ina uwezo wa hali ya juu katika suala zima la kupiga self na kwamba ni simu ya kijanja inayoendana na kasi ya mabadiliko ya Teknlojia ya simu.


Akizindua simu hiyo meneja mauzo toka Tekno Fredy Kadelane amesema simu hiyo imekuja kukidhi haja ya wateja wanaotaka vitu vyenye viwango vya juu, akisistiza simu hiyo kuwa ni Zaidi ya simu.


“Kama mpenzi wa picha Camon C9 imekupa Camera unayoihitaji kwani inaweza kutambua sura na kupiga selfie kali hata ukiwa gizani. Pia Camera yake ina urembo wa kweli (make-up) ambayo itafanya picha zako kuwa na mvuto wa asili.” Alisema Kadelane

Ameongeza kusema Tecno Camon C9 ina uwezo wa kujaza watu wengi kwenye selfie moja jambo ambalo ni tofauti na simu yoyote ile duniani. Camera ya C9 inachukua angle kubwa zaidi hivyo kukuwezesha kupata selfie nzuri ya watu wengi zaidi. 


Ametaja sifa nyingine ya Simu ya Camon C9 kuwa ina Iris recognition Inayosaidia mmiliki wa simu kuweza kufunga simu yake na kufungua kwa njia ya kuitazama badala ya kuweka neno la siri (Password) kama ilivyozoeleka katika simu zingine.


“Sasa hakutokuwa na sababu ya kuweka password, Tecno inatumia teknolojia mpya ya IRIS recognition ambayo inatumia macho kufungua simu. “ alisema


WATEJA 100 WA KWANZA WAPEWA SIMU ZAO


Aidha wateja 100 wa kwanza ambao walifanya zoezi la ku order mapema simu hizo wamefanikiwa kupewa simu zao katika showroom ya Tecno iliyopo duka la City Mall jijini Daresalaam.


“Uzinduzi huu unaenda sambamba na kutoa simu kwa wateja wetu miamoja wa kwanza waliyofanya manunuzi ya awali (pre-order) katika show room zetu zilizopo City Mall, Clock tower na Mobile plaza ghorofa ya pili.”Alisema 


Aidha akifafanua jinsi wateja wa awali walivyoshiriki kufanya manunuzi ya awali, Amesema wateja hao walifanya malipo ya awali ya Tsh. 30,000 na kupewa kadi ya “huduma kwa wateja kutoka” Tecno na kifurushi cha zawadi (gift hamper) za bidhaa kutoka Tecno. 


Kadi ya huduma kwa wateja itatumika katika kutengenezewa simu katika duka zetu za Tecno baada ya kujipatia simu yenyewe. 


WATEJA WAIPA KONGOLE TECNO MOBILE


Kwa upande wao wateja waliofika katika duka la city mall kuchukua simu zao hawakusita kuonyesha furaha yao baada ya kupokea simu hizo wakisema simu hizo zinaendana na wakati wa sasa na kwamba gharama yake ni nafuu ukilinganisha na ubora wa simu yenyewe.


Akizungumza na Fullhabari.com, mmoja wa wateja hao Bw.Harrison Ndungulile amekili kwa kusema simu hiyo ya common c9 imekuja kukidhi haja za watu wanaopenda zimu za smartfone

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...