Skip to main content

KIJIJI CHA LUDILO WAPITISHA SHERIA NDOGO ZA USIMAMIZI WA MALIASILI









Wananchi wa kijiji cha Ludilo wilayani Mufindi, mkoani Iringa wamepitisha sheria ndogo ya usimamizi wa maliasili (misitu na wanyamapori) ilikukabiliana na kasi ya uharibifu wa rasilimali hizo.

Hatua hiyo ilifikiwa tarehe 4 Augusti, 2016 katika mkutano wa hadhara ambapo Diwani wa kata ya Mdabulo Mheshimiwa Henry Nyeho pamoja na Mwanasheria wa Wilaya ya Mufindi Leonard Jaka walihudhuria mkutano huo.


Sheria zilizopitishwa na wananchi hao ndio itakayotumika katika usimamizi wa maliasili.

Mchakato wa uboreshaji sheria ulianza mwezi Juni, 2016 ambapo Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) kwa kushirikiana na Mwanasheria wa Wilaya ya Mufindi pamoja na wananchi hao, kupitia mkutano wa hadhara waliangalia upya sheria zilizokuwa zikitumika kijijini hapo na kugundua kuwa zilikuwa na mapungufu. 


Wananchi wakiongozwa na Wanasheria kutoka LEAT na Mwanasheria wa Wilaya Mufindi walitoa mapendekezo ya maboresho na kuiruhusu timu ya LEAT kuchapisha sheria hizo mpya ambazo ziliwasilishwa tarehe 4 August 2016. 



Mtendaji wa kijiji cha Ludilo Martin Mwanule alisoma kipengele kimoja baada ya kingine kupitishwa na wananchi. 


Sheria hizo zinaelekeza haki na wajibu wa wananchi, serikali ya kijiji, kamati ya maliasili pamoja na timu ya Ufuatiliaji Uwajibikaji Jamii. Pia sheria zimefafanua adhabu zitakazotolewa kwa watu watakao kiuka sheria na kuharibu maliasili. 

Hii ni awamu ya kwanza ya kuzijengea uwezo serikali za vijiji wa kuunda sheria ndogo za kusimamia maliasili. 



Katika awamu hii vijiji vya Ludilo, Ikangamwani na Kibada kwa wilaya ya Mufindi. Kwa wilaya ya Iringa ni vijiji vya Mbweleli, Kinyika na Kinyali.


Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) inatekeleza mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili katika vijiji 32 vya wilaya za Iringa na Mufindi mkoani Iringa.

Mradi huu umefadhiliwa na Watu wa MArekani kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo la MArekani (USAID). 

Lengo la mradi ni kuzijengea uwezo jamii zinazoishi karibu na rasilimali misitu na wanyamapori, iliwaweze kuzisimamia na kunufaika nazo. 

Mradi unatoa mafunzo ya sheria, sera, miongozo, kanuni na Ufuatiliaji uwajibikaji jamii kwa kamati za vijiji za maliasili na mazingira, uchumi, maji na matumizi ya ardhi. 

Pia mradi umetoa mafunzo kwa wananchi, madiwani na asasi za kiraia. Takriban wananchi 6500 watafikiwa na mafunzo hayo. 

Katika kutimiza azma ya kutoa elimu ya usimimizi wa maliasili kwa wananchi wengi, LEAT inatoa mafunzo kwa njia ya redio, sambamba na kutoa elimu kwa njia ya sanaa kupitia kikundi cha Sanaa Mashujaa kwa wilaya ya Iringa na kikundi cha Sanaa Mapogoro kwa wilaya ya Mufindi.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...