Skip to main content

N/WAZIRI JAFO: WATANZANIA WANAPASWA KUTHAMINI BIDHAA ZINAZOZALISHWA NCHINI


Naibu waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Jafo Suleiman Said akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama mara baada ya kutembelea banda la Halmashauri hiyo.




Mgeni na Mwenyeji wakifurahi kufuatia maandalizi mazuri ya Maonesho ya Nane nane kanda ya kati.




Naibu waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Jafo Suleiman Said akisikiliza maelezo ya namna ya kulima kilimo na ufugaji wa kisasa




Na Mathias Canal, Dodoma

Watanzania wametakiwa kuthamini na kununua bidhaa zinazozalishwa nchini Tanzania hususani katika sekta ya Kilimo, Ufugaji na uvuvi kwani hakuna sababu ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi ilihali bidhaa hizo wanazoagiza zinazalishwa na watanzania wenzao.

Naibu waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Jafo Suleiman Said ameyasema hayo mara baada ya kutembelea baadhi ya mabanda katika maonyesho ya wakulima Nane nane Kanda ya kati Dodoma yanayofanyika katika uwanja wa Nzuguni huku kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni "Kilimo, Mifugo na Uvuvi ni nguzo ya maendeleo, Kijana shiriki kikamilifu (Hapa Kazi Tu).

Jaffo amesema kuwa asilimia kubwa ya watanzania wamekuwa watumwa wa mambo ya kigeni, kuiga tamaduni mbalimbali ikiwemo matumizi ya bidhaa zinazotoka nje ya nchi wakati pia bidhaa hizo zinazalishwa nchini, huku akitolea mfano wa manunuzi ya viatu kutoka nchi mbalimbali wakati hapa nchini Jeshi la Magereza linatengeneza viatu bora vya ngozi tena kwa bei nafuu.

Sambamba na hayo pia Naibu Waziri huyo ameiagiza Mamlaka ya Ustawishaji Makao makuu Dodoma kusimamia vyema na kwenda na kasi kubwa katika utengenezaji wa stendi kubwa na ya kisasa ili kufanana na mji wa Dodoma ambapo pia hivi karibuni makao makuu ya serikali yatahamia mjini hapo.

Aidha ameongeza kuwa Maonesho hayo yanapaswa kuboreshwa ili maonyesho yajayo yawe ya kitaifa ambapo nchi mbalimbali zitapata fursa ya kutembelea na kuifanya Tanzania kujikomboa katika wimbi la umasikini.

Maonesho hayo yanahusisha Shughuli za wakulima, wafugaji wa mifugo, wafugaji wa nyuki, wavuvi, wana mazingira, wasindikaji wa bidhaa za mazao ya kilimo na mifugo, wizara taasisi/Makampuni ya umma, makampuni Binafsi, mabenki, taasisi za umma na za binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali.

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya waandaaji wa Maonesho hayo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Miraji Jumanne Mtaturu amesema kuwa maandalizi ya maonyesho hayo yametumia muda mfupi lakini kwa kiasi kikubwa yamekuwa bora na kuahidi kuwa na Maonesho yajayo kuwa bora zaidi katika kipindi kinachokuja.

Mtaturu amesema kuwa lengo mahususi la maonesho hayo ni utoaji wa elimu ya matumizi ya teknolojia mbalimbali kwa wadau wengi kwa muda mfupi ambapo watajifunza kwa njia ya kuona, kujadiliana na kuulizana maswali.

Ameongeza kuwa maeneo makuu ya mafunzo ni teknolojia za uzalishaji wenye tija wa mazao, mifugo na usindikaji wa bidhaa ili kuongeza thamani.

Dc Mtaturu amesema kuwa pia wadau watajionea na kujifunza huduma zitolewazo na serikali, Mashirika ya umma na binafsi, ambapo wafanya biashara wanayatumia maonesho hayo kwa kuuza bidhaa, kufahamiana na kuingia makubaliano.

Kwa upande wake Katibu wa maandalizi ya Maonesho hayo Aziza Rajabu Mumba amesema kuwa Wanatarajia kila mwananchi atakayetembelea maonesho hayo kwenda kutekeleza kwa vitendo anayojifunza katika eneo lake na kuwafundisha wengine ambao hawakupata fursa ya kuhudhuria kwenye Maonesho hayo.

Aidha amesema Malengo ya muda mrefu ni kuendeleza uwanja wa Nzuguni ufikie ubora na hadhi ya viwanja vya maonesho ya Kilimo Kimataifa na kuendelea kushawishi wadau mbalimbali kuwekeza ili kuufanya uwanja wa Nzuguni uwe kituo cha huduma cha Maonesho ya Kilimo nchini kama ilivyo kwa uwanja wa Mwalimu Nyerere Dar es salaam kwa maonesho ya Biashara.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...