Skip to main content

TIGO YAANZISHA KIFURUSHI KIPYA MAHSUSI CHA MIITO NA DATA KATIKA TAMASHA LA FIESTA 2016





Meneja Chapa wa Kampuni ya Simu ya Tigo, William Mpinga (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya Kampuni hiyo, Kijitonyama Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu kampuni hiyo kuanzisha kifurushi kipya mahsusi cha miito na data katika tamasha la Fiesta 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa Tamasha la Fiesta, Sebastian Maganga.




Mwenyekiti wa Tamasha la Fiesta, Sebastian Maganga (kushoto), akizungumzia kukamilika kwa maandalizi ya tamasha hilo.


Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.


Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya simu ya Tigo imetangaza vifurushi viwili vipya vya miito na data vinavyofahamika kama ‘Vifurushi vya Fiesta’ (Fiesta packages) ambavyo vinalenga kuwanufaisha watega wote wa Tigo na wasio wakati wa tamasha la Fiesta 2016.

Vifurushi hivi vya kuvutia vitakuwa vinapatikana kwa wateja wote watakaohudhuria matamasha na hata wasio hudhuria.

Vifurushi vipya vitawawezesha wateja kuchagua kati ya data za GB 1 au visivyo na ukomo ambavyo vinajumuisha dakika 490 Tigo kwenda Tigo, dakika 10 mitandao yote na SMS 100 kwa shilingi 1000 wakati wale ambao sio wateja wa Tigo ambao wamenunua kadi ya simu ya 4G ya Tigo watapata dakika 60, sms 60 na MB 60 papo hapo pindi wanapojisajili na baadaye kuchagua kati ya data na kifurushi kisicho na ukomo.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari katika makao makuu ya Tigo, Meneja Chapa, William Mpinga alisema, “vifurushi hivi vimekuwa ikiwa ni ahadi tulioyoitoa kwa wateja wetu kuhusu ofa mbalimbali na promosheni ambazo zitakuwepo wakati wa msimu wa Fiesta 2016. Hali kadhalika tutaendelea na uanzishaji wa bidhaa na huduma za ubinifu ili kukidhi mahitaji ya wateja wetu na pia kutoa nafasi kwa wateja wapya.”

Mpinga alifafanua kuwa tamasha la Fiesta 2016 linawakaribisha Watanzania wote na kuongeza kuwa pia tukio hilo litatoa shughuli zenye mabadiliko kijamii.

Mpinga alisema, “Mwanzoni wa wiki iliyopita tulianzisha kauli mbiu ya tamasha la fiesta inayosema, "Fiesta 2016 Kwa Kishindo cha Tigo, Imooooo!" ambapo mantiki iliyopo katika kauli mbiu hii ni kutoa bidhaa na huduma ambazo ni mahsusi kwa wateja wetu katika kipindi cha tamasha.”

Mwenyekiti wa Tamasha la Fiesta 2016, Sebastian Maganga alisema, “ Tunafurahi sana kutangaza kwamba tamasha la Fiesta 2016 litaanza rasmi jijini Mwanza Agosti 20, 2016. Kwa hiyo wakazi wa Mwanza na vitongoji vyake watarajie kupata vifurushi hivi maalum pamoja na shughuli za kufurahisha katika kipindi cha wiki nzima kabla ya tamasha.”

Tamasha la Fiesta 2016 linaandaliwa kila mwaka na kampuni ya Prime Time Promotions, na hivi sasa ni mwaka wa 15 tangu kuanziswhwa kwake na linatarajiwa kujumuisha mikoa 15 ambayo ni pamoja na Mwanza, Kahama, Kagera, Musoma, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Morogoro, Tanga, Kilimanjaro, Mtwara, Iringa, Mbeya na Dar es Salaam.

Tamasha la Fiesta 2016 linafanyika kwa ushirikiano wa Prime Time Promotions na Tigo Tanzania ambayo ni mdhamini mkuu.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...