Skip to main content

DC IKUNGI AITAKA KAMPUNI YA SHANTA GOLD MINE KUWALIPA FIDIA WANANCHI WALIOFANYIWA TATHIMINI



Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza wakati wa kikao cha pamoja kilichohudhuriwa na Wawakilishi wa kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi


Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi wakijadili jambo nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya kabla ya kuingia kwenye kikao


Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd Philbert Rweyemamu akielezea namna ambavyo watawalipa wananchi 67 ndani ya wiki hii






Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi wakisikiliza kwa makini maelezo ya mkuu wa Wilaya 




Kamishina wa Madini Kanda ya Kati Sospita Masorwa akielezea namna ambavyo uthamini unakuwa umekamilika kuwa ni mara baada ya Mthamini Mkuu wa serikali kupitisha


Kutoka kushoto ni Afisa Tarafa ya Ikungi Josephine, Kamishina wa Madini Kanda ya Kati Sospita Masorwa, Ally Kassim Mjiolojia kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Meneja Mkuu Shanta Gold Mine Ltd Philbert Rweyemamu, David Rwechungura Meneja Rasilimali watu kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, na Daniel Mwita



















Na Mathias Canal, Singida


KAMPUNI ya Uchimbaji wa Madini ya dhahabu (Shanta Gold Mining Limited) iliyopo katika kijiji cha Sambaru Kata ya Mang’onyi Wilayani Ikungi, Mkoani Singida imetakiwa kuwalipa wananchi 69 waliosalia kulipwa fidia zao kwa ajili ya kupisha mradi wa uchimbaji dhahabu.


Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kufuatia malalamiko ya wananchi wa maeneo mbalimbali waliopo kwenye eneo la mradi huo waliotaka kufahamu hatima ya malipo yao kutokana na awamu ya kwanza kuonyesha kuwa watu 67 ndio watakaolipwa mwishoni mwa wiki hii na wengine waliobaki kulipwa katika awamu zijazo.


Dc Mtaturu ametoa agizio hilo wakati wa kikao cha pamoja kilichohudhuriwa na Wawakilishi wa kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi ambacho kilipewa jukumu la kuhakikisha wananchi wote ambao watapitiwa na mradi huo wanalipwa fidia sambamba na kusimamia uhamishaji wa makazi.


Kapuni ya Shanta Gold Mine ltd imetakiwa kutumia siku 68 yaani hadi kufikia mwezi Novemba mwaka huu kumaliza malipo ya watu 69 kati ya 136 ambao wanatakiwa kulipwa katika awamu ya pili ili wananchi hao waweze kupisha mradi huo ambao kwa kiasi kikubwa umeshindwa kuanza uchimbaji wa madini aina ya dhahabu kutokana na malalamiko ya malipo ya fidia kwa baadhi ya wananchi ambao tayari wamefanyiwa uthamini wa maeneo yao.


Sambamba na hayo pia Mkuu huyo wa wilaya ameagiza kikosi kazi kuendeleana kazi yake mpaka pale malipo ya wananchi hao yatakapokamilika pamoja na kuwapo kwa maneno kuwa kilivunjwa mwanzoni mwa mwezi wa tatu, jambo ambalo limepingwa vikali na uongozi huo wa Wilaya.

Kwa upande wake Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd Philbert Rweyemamu amesema kuwa kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi hao juu ya kutaka wananchi wote walipwe kwa wakati mmoja jambo ambalo sio rahisi kutokana na pesa iliyopatikana kutoka kwa wawekezaji wa hisa tangu mwaka 2012 mpaka sasa bado inatumika haijaanza kuingiza faida hivyo malipo ya awamu yatakuwa muarobaini wa malipo hayo mara baada ya kuanza kwa uchimbaji hivyo kadri mradi unavyoendelea kuchelewa kuanza ndivyo ambavyo fedha inapoteza thamani.


Hata hivyo amejibu hoja ya wananchi kuwa Kampuni hiyo ndiyo ilileta Mthamini wa maeneo ya wananchi jambo ambalo halina ukweli halisi kwani wananchi wenyewe ndio walioamua juu ya Mthamini wanayemtaka kutokana na makubaliano yao.


Rweyemamu alisema kuwa endapo kama mradi huo ungeanza mapema kama vile ilivyokuwa imepangwa ni dhahiri sasa ungekuwa umezalisha ajira zaidi ya mara tano kwa wakazi wa maeneo husika na Taifa kwa ujumla jambo ambalo lingerahisisha kuongeza pato la wananchi wa Wilaya husika na Taifa kwa ujumla.


Naye Mwenyekiti wa wananchi walio katika eneo la mradi huo Ramadhani Said Nyeri amesifu juhudi za utendaji kazi wa serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kumteua Mkuu huyo wa Wilaya ambaye anaonyesha maslahi mapana na wananchi kutokana na juhudi mbalimbali za utendaji kazi.


Pamoja na pongezi hizo Nyeri amesema kuwa endapo viongozi mbalimbali wa serikali watafanya kazi kwa mazoea kwa kutumia vibaya nafasi zao ni dhahiri kuwa lawama na malalamiko ya wananchi yatakuwa laana kwao.

Nyeri alisema kuwa kikosi kazi hicho kilianza kazi hiyo mwaka 2014 ambacho kilianzishwa na Kampuni ya Shanta gold Mine ltd kwa makubaliano na wananchi wa maeneo husika ambapo katika kipindi chote hicho vimefanyika vikao vitano ambavyo viliendeshwa vyema pasina malalamiko kwa upande wowote ule.


Akifunga kikao hicho Dc Mtaturu alisema kuwa katika makubaliano ya namna ya kuendesha utendaji kazi wa kikosi kazi hicho mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Tundu lissu alipaswa kuwepo lakini hajawahi kushiriki hata kikao kimoja jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linaashiria mbunge huyo kukimbia majukumu yake kama muwakilishi wa wananchi.






Aidha amekipongeza kikosi kazi hicho kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya kwa kipindi chote hicho huku akiitaja miaka 10 waliyofanya kazi kumekuwa na daraja kutokana na baadhi ya viongozi kukimbia majukumu yao na kuwaacha wananchi kujishughulikia na kumaliza matatizo yao wao wenyewe.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...