Skip to main content

DC STAKI APONGEZA JAMII YA KIMASAI KUACHANA NA MILA POTOFU




Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule akisikiliza kwa makini maelezo ya mmoja ya wazee wa kabila la Kimasai kuhusu umuhimu wa elimu katika maeneo hayo




Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule, Viongozi wa dini na wananchi wakishuhudia sherehe ya vijana wa kimasai (Morani) kuingia stage ya uzeeni 




Baadhi ya vijana wa Kimasai wakipandisha Mori kwa furaha ya kuingia stage ya uzee






Dc Staki akisalimiana na viongozi wa dini walioendesha misa hiyo mara baada ya kuwasili katika viwanja hivyo





Dc Staki akishuhudia vijana wakipandisha Mori




Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Rosemary Staki Senyamule akiwa kwenye sala wakati wa Misa



Dc Staki akifatilia kwa makini zoezi la kuingia hatua ya Uzee kwa waliokuwa vijana wa Kimasai
Na Mathias Canal, Kilimanjaro


Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Rosemary Staki Senyamule amewapongeza baadhi ya vijana wa kimasai kwa kuachana na imani potofu na hatimaye kuanza kumwabudu Mungu kwa kuhudhuria Misa mbalimbali katika makanisa.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu huyo wa Wilaya hiyo wakati wa sherehe maalumu kwa waliokuwa vijana wa Kimasai (Morani) kuingia hatua kubwa ya uzeeni na ya heshima katika kabila hilo.

Sherehe hiyo ilifanyika katika uwanja wa Kitongoji cha Endevisi, Kijiji cha Emuguru na ibada hiyo kuongozwa na Mchungaji Joshua Laiser kutoka kanisa la Kiinjili la kilutheli Tanzania (KKKT) Wilaya ya Hai Dayosisi ya Moshi na Mchungaji Andrea Sangolo wa Usharika wa Bonde la Ruvu Same na baadaye kufuatiwa na shughuli za kutoa Baraka kwa vijana hao zoezi lililofanywa na viongozi wa dini, Serikali na Wazee wa Mila.

Sherehe hizo zimefanyika zikiwa na lengo la kufanya mageuzi kwa jamii ya kimasai na hatimaye kuachana na mila potofu kama vile kuabudu waganga wa jadi na kuanza kumuabudu Mungu wa kweli.

Pamoja na pongezi hizo za mkuu wa Wilaya ya Same kwa jamii ya kimasai kufanya mapinduzi hayo ya kuachana na mila potofu pia aliwataka kuwekeza zaidi kwenye swala la elimu na kuwataka kuwaruhusu watoto wote wa kiume na watoto wa kike kusoma kwa usawa.

Katika Jamii ya kimasai kumekuwepo na kadhia mbalimbali za mila Potofu za kuozesha watoto wadogo na kufanyiwa tohara kwa watoto wa kike, matukio ya ubabe ikiwemo wizi wa mifugo na mauaji kwa imani potofu jambo ambalo limezuiwa na Mkuu huyo wa Wilaya hiyo.

Dc Staki ametumia nafasi hiyo pia kuwataka wananchi wote wa jamii hiyo ya Kimasai kutumia rasilimali walizo nazo kwa kuuza kiasi ikiwemo Ng’ombe ili kujenga Hospitali zitakazo wasaidia kuimarisha afya zao na kujenga shule ambazo zitawaimarisha watoto wao kielimu.

Tukio hilo la Ibada kwa vijana hao ni kubwa katika historia ya kabila la Kimasai na limejumuisha jamii ya Kimasai kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Tanzania na nchi jirani ya Kenya.






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...