Skip to main content

UZINDUZI WA KONDOM MPYA YA ZANA WAFANYIKA MKOANI MWANZA



Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi (kushoto) akizindua Kondom mpya ya Zana inayotolewa na Serikali bure kwa wananchi kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi.


Kondom ya Zana ni mbadala wa kondom iliyokuwa ikitolewa pia bure na serikali na kusambazwa na Bohari ya Dawa nchini MSD ambapo kondom hiyo haikuwa na jina, rangi na kifungashio chenye kuvutia hali ambayo ilisababisha wananchi kudhania kwamba haina ubora jambo ambalo hata hivyo halikuwa sahihi kwani ilikuwa na ubora kama aina nyingine za kondom.




Uzinduzi wa Zana Kondom mkoani Mwanza






Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, amesema kumekuwa na dhana potofu kwa wananchi kuhusu kondom zinazotolewa bure na serikali kwamba hazina ubora jambo ambalo siyo sahihi ambapo amewahahikikishia kwamba kondom ya Zana ina ubora wa hali ya juu hivyo ni vyema wakazingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom hiyo ili kuondokana na magonjwa ya zinaa na mimba zisizotarajiwa. 


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi, amebainisha kwamba serikali imekuwa ikitumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuwahudumia wanaoishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi hivyo ni vyema wakazingatia matumizi ya kondom ili kujikinga na maambukizi hayo.


Dr.Pius Masele ambaye ni Mratibu wa Ukimwi mkoa wa Mwanza, akizungumza na wanahabari ambapo amesema hali ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi ni asilimia 4.2 na kwamba serikali inaendelea kuhakikisha kwamba inatomeza mambukizi hayo pamoja na magonjwa mengine ya ngono kwa kuhamasisha wananchi kuzingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom


Kutoka kushoto ni Dr.Pius Masele, Mratibu wa Ukimwi mkoani Mwanza, Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dr.Leonard Subi, Mratibu wa TACAIDS mkoani Mwanza, na Mratibu PSI mkoani Mwanza, Clement Mbogo.


Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, akizungumza kwenye uzinduzi huo.


Dr.Pius Masele, Mratibu wa Ukimwi mkoani Mwanza, akizungumza kwenye uzinduzi huo


Mratibu PSI mkoani Mwanza, Clement Mbogo, akizungumza kwenye uzinduzi huo wa Zana Kondom mkoani Mwanza


Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dr.Leonard Subi, akizungumza kwenye uzinduzi wa Zana kondom mkoani Mwanza


Taswira Ukumbini


Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa kondom ya Zana mkoani Mwanza



Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa kondom ya Zana mkoani Mwanza



Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi, amebainisha kwamba serikali imekuwa ikitumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuwahudumia wanaoishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi hivyo ni vyema wakazingatia matumizi ya kondom ili kujikinga na maambukizi hayo.


Amesema ili kuondokana na matumizi hayo ya fedha, Serikali inawahimiza wananchi kuzingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom, ili kuondokana na maambukizi ya virusi hivyo pamoja na maambukizi mengine ya magonjwa zinaa ikiwemo kaswende.


Dr.Subi ameyasema hayo hii leo kwenye uzinduzi wa kondom mpya ya Zana uliofanyika mkoani Mwanza, ambayo itakuwa ikisambazwa bure kwa wananchi na serikali ili kusaidia wananchi kuondokana na magonjwa ya zinaa pamoja na kimba zisizotarajiwa.

Amesema ni vyema wananchi wakaendelea kuhimizwa kuwa na matumizi sahihi na endelevu ya kondom ya Zana, hatua itakayosaidia kupunga ongezeko la waathirika wa magonjwa ya zinaa ikiwemo virusi vya Ukimwi na hivyo kuipunguzia serikali matumizi makubwa ya fedha kwa ajili ya kuwahudumia wenye maambukizi hayo.

Naye Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, amesema kumekuwa na dhana potofu kwa wananchi kuhusu kondom zinazotolewa bure na serikali kwamba hazina ubora jambo ambalo siyo sahihi ambapo amewahahikikishia kwamba kondom ya Zana ina ubora wa hali ya juu hivyo ni vyema wakazingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom hiyo ili kuondokana na magonjwa ya zinaa na mimba zisizotarajiwa.

Uzinduzi wa kondom mpya ya Zana inayotolewa bure na serikali kwa wananchi, ulifanyika Kitaifa Agosti 30,2016 mkoani Mbeya ambapo kwa mkoa wa Mwanza umefanyika hii leo Jijini Mwanza ambapo wahamasishaji rika watakuwa wakipita mitaani kuwahamasisha wananchi juu ya matumizi sahihi ya kondom hiyo na baadae uzinduzi kama huo utaendelea katika mikoa mingine nchini lengo likiwa ni kuwahamasisha wananchi kutumia kondom hiyo ili kusaidia mapambano dhidi ya magonjwa ya zinaa ikiwemo virusi vya Ukimwi na mimba zisizotarajiwa.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...