Skip to main content

Vijana nchini wahimizwa kuunga mkono kampeni ya Uchumi wa Kijani


Mkutano Vijana na Uchumi wa Kijani






Baadhi ya picha kutoka katika mkutano huo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Raleigh Tanzania, Bw Alistar Mackay akizungumza na washiriki wa mkutano


Washiriki wa mkutano huo
Wawakilishi wa taasisi na ofisi za serikali

Mgeni Rasmi akizungumza na waandishi wa habari
Ms Clara Makenya kutoka United Nations Environment Programme akizungumzia uchumi wa kijani katika mkutano huo.




Vijana nchini Tanzania wahimizwa kujiunga na kampeni ya Vijana kwa Maendeleo ya Kijani ili kulinda mazingira kwa kuyafanya endelevu sambamba na kujiiinua kiuchumi.

Hayo yalibainishwa na Afisa Mawasiliano wa shirika la kimataifa la Raleigh Tanzania Bw. Kennedy Mmari wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kampeni ya Uchumi wa Kijani kwa Vijana iliyofanyika kwatika ukumbi wa British Council.

Bwana Mmari alisema kuwa wao kama shirika linalojihusisha na vijana wamekuja na kampeni hii ya kitaifa kwakua wanaamini uwezo walionao vijana katika kuleta mabadiliko endapo watapewa nafasi.

 “Sisi kama vijana tunahitaji sana maendeleo ya kiuchumi ila lazima maendeleo hayo yalinde mazingira yetu hivyo basi tunahitaji uchumi wa kijani, uchumi ambao utazingatia vilivyo shughuli za kiuchumi kwaajili ya kupunguza umasikini lakini ukijikita pia katika kuhakikisha kuwa kunakuwepo na mazingira endelevu” alielezea Bw. Mmari.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Raisi  Muungano na Mazingira Injinia Ngosi Mwihava alisema wao kama Serikali wametoa Baraka zote kwa kampeni hiyo kwani athari za mabadiliko ya tabia nchi zimedi kuongezeka siku hadi siku.


“Sisi kama serikali ni jukumu letu kuhakikisha wananchi wanayatunza mazingira na kuyafanya yawe endelevu, na ndio maana leo tupo hapa na vijana ili kuhakikisha elimu ya mazingira endelevu inawafikia na wao wanaisambaza” alisema Injinia Mwihava.

Aidha Injinia Mwihava alisema kuwa serikali itahakikisha mazingira yanalindwa na kuwa endelevu hivyo wataanza na kupiga marufku matumizi ya mifuko ya plastiki kuanzia Januari mwakani kama njia mojawapo wa kuzuia uchafuzi wa mazingira.

“Serikali sasa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tunaandaa kanuni  za kudhibiti mifuko ya plastiki nchini na hata kama mgeni akija nayo toka nje akifika mpakani lazima aambiwe kuwa hatutumii tena mifuko ya plastiki” alisisitiza Injinia Mwihava.

Naye mmoja wa vijana waliohudhuria hafla hiyo Pius Matunge  alisema ni wakati sasa kwa vijana kushika hatamu kwenye kulinda mazingira.
"Kila kijana lazima ajione yuko mbele kwenye kulinda na kuyatetea mazingira ili yaweze kutumika kwenye kuinua uchumi wa nchi yetu" alihitimisha Bw. Pius.


Hafla hiyo iliyoandaliwa na shirika Raleigh Tanzania ilikutanisha pamoja vijana kutoka mikoa mbalimbali nchini na mashirika mbalimbali na wadau wa mazingira kujadili jinsi gani vijana wanaweza kuwa mawakala wa maendele ya Uchumi wa Kijani.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...