Skip to main content

Watanzania watakiwa kutunza mazingira




Na Rabi Hume, MO BLOG


Kutokana na kuwepo na shughuli nyingi za kibinadamu ambazo zinaharibu mazingira, watanzania nchini kote wametakiwa kuwa makini kwa kutunza mazingira yanayowazunguka ili kuepusha matatizo ambayo yanaweza kutokea kutokana na kushindwa kudhibiti vitendo vya uharibifu mazingira.


Rai hio imetolewa na Balozi Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa Geneva, Uswisi, Modest Mero katika warsha ya kujadili kuhusu kilimo na biashara iliyoandaliwa na Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF).


Balozi Mero alisema kuwa nchi nyingi duniani zimekuwa na shughuli nyingi ambazo zinaharibu mazingira hali ambayo inatishia maisha ya vizazi vijavyo na hivyo ni vyema watanzania wakaanza kuchukua hatua kwa kutunza mazingira ili kuepeusha athari ambazo zitajitokeza kwa miaka ijayo.


"Dunia nzima watu wanakata miti, wanachoma majani mashambani lakini hawajui kama kuna vitu vya muhimu wanaua ardhini, na mimi niwambie watanzania wawe makini wasikate miti ambayo inawazunguka huo ni uharibifu wa mazingira," alisema Balozi Mero.


Balozi Mwakilishi wa Mashirika ya Kimataifa Geneva, Uswisi, Modest Mero akizungumza na washiriki wa warsha iliyoandaliwa na Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), ikizungumza kuhusu kilimo na biashara. (Picha zote na Rabi Hume - MO BLOG)


Aidha alisema kuwa kwa sehemu kubwa watu ambao wanachangia vitendo hivyo ni wafanyabiashara na hivyo kuwataka wafanyabiashara kuacha vitendo vya kukata miti ikiwa bado haijafika katika muda sahihi ambao wanaruhusiwa kuikata.


"Wafanyabiashara wanakata sana miti, lakini wajue kuwa wakikata hovyo baadae wataikosa hiyo miti, ili mazingira yanayotuzunguka yawe mazuri inabidi kuyatunza ila tukitumia vibaya hata vyanzo vya maji vitakauka," alisema Mero.


Mtafiti Mshiriki wa ESRF, Dkt. Osward Mashindano akizungumzia malengo ya warsha hiyo.


Nae Mtafiti Mshiriki wa ESRF, Dkt. Osward Mashindano alisema warsha hiyo ina lengo la kuzungumzia jinsi gani kilimo, biashara, usalama wa chakula na mabadiliko ya hali ya nchi jinsi ambavyo vinaweza kutoa matokeo mazuri au mabaya.


Alisema kuwa pamoja na matokeo hayo, pia wanazungumzia ni hatua gani inafaa kuchukuliwa iwapo matokeo yanakuwa ni mazuri au mabaya ili kumsaidia mkulima mdogo kwa jinsi gani anaweza kufaidika na kilimo chake na kuepuka kupata hasara.


"Bidhaa kwa sasa zinatakiwa kuongezwa thamani, bidhaa kama haijaboreshwa haiwezi kuwa na soko zuri la ndani na hata nje ya nchi, tunataka kujua matokeo yake yanakuwaje maana biashara inavutia kutokana na soko lake lilivyo,


"Watu wanatakiwa kujua matokeo kama ni mazuri wafanyaje kama wengine wanaweza wanachangamkia fursa au kama ni mabaya wajue jinsi gani wanaweza kupunguza athari hizo ... tunatazama hilo maana hata sera zilizopo sasa hazisemi hatua gani ichukuliwe kama matokeo ni mabaya au mazuri," alisema Dkt. Mashindano.




Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wakihangia mada zilizokuwa zikijadiliwa.



Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...