Skip to main content

HOSPITALI MKOA WA IRINGA KUENDESHA KLINIKI YA KUPIMA KISUKARI NA SHINIKIZO LA DAMU




Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa itaendesha Kliniki ya kupima ugonjwa wa Kisukari na Shinikizo la Damu kwa wananchi wa Manispaa ya Iringa na maeneo yanayozunguka Manispaa hiyo. 

Kliniki hiyo itazinduliwa tarehe 10/11/2016 na itaendelea kwa siku tano mfululizo hadi tarehe 14/11/2016 siku mbayo ni kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kisukari Duniani.

Akizungumza na SIMBAYABLOG leo (Jumatano) Afisa wa Habari Mkoa wa Iringa Dennis Gondwe, alisema huduma za upimaji zitafanyika katika Bustani ya Manispaa ya Iringa kuanzia saa 2:00 Asubuhi hadi saa 10.30 Jioni kila siku, na kuongeza kuwa huduma zote zitatolewa bure.

Siku ya Kisukari Duniani ilianzishwa mwaka 1991 na Mashirika mawili ya kimataifa yaani World Health Organization (WHO) na International Diabetes Federation (IDF) baada ya kuona ugonjwa wa Kisukari unaongezeka sana Duniani na Siku hiyo huadhimishwa Duniani kote kila mwaka ifikao tarehe 14 Novemba. 

Alisema kuwa Mkoa wa Iringa kama maeneo mengine Duniani unaadhimisha siku hii, kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kupima wananchi wake ili waweze kufahamu hali zao na pia kutoa elimu ya umuhimu wa kuzuia na kujikinga na madhara yatokanayo na ugonjwa wa kisukari.

Ugonjwa wa Kisukari ni hali ambayo hutokea wakati sukari katika damu inapokuwa nyingi kupita kiwango cha kawaida kwa muda mrefu. 

Sukari hutumiwa na mwili ili kupata nishati lishe. Ili mwili uweze kutumia sukari inayotokana na vyakula, unahitaji kichocheo cha insulin. 

Insulin husaidia sukari kuingia kwenye chembechembe hai ili kutengeneza nishati lishe. Ugonjwa wa kisukari unasababishwa na kichocheo hiki kupungua au kutofanya kazi kama inavyotakiwa.

Hivyo kiwango cha kisukari kinabaki kikubwa kwenye damu kwa sababu sukari haikuwezeshwa kuingia kwenye chembechembe hai za mwili.


“Mara nyingi, watu wengi hawajitambui kuwa wana ugonjwa huu. Wengine wanakuwa na dalili lakini hawachukui hatua mapema,” alisema Gondwe. 

Alisema kuwa dalili za kisukari ni rahisi kuzitambua. Dalili hizo ni: kiu isiyoisha, kukojoa mara kwa mara, kupungua uzito, kusikia njaa kila wakati na mwili kukosa nguvu. Mwananchi yeyote akiwa na dalili hizi aende hospitali au katika kituo cha Afya ukapime sukari. 

Hata hivyo, afisa habari huyo ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Iringa kuzingatia ulaji unaofaa wa vyakula. 

Aliseam kuwa ulaji unaofaa ni kula chakula mchanganyiko cha kukutosha kukua na kuwa na uzito wa kawaida na chenye virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini. 

Kwa mfano vyakula vya wanga vinasaidia kuupa mwili nguvu na joto, protini husaidia kujenga mwili na kutengeneza vichocheo mbalimbali, vitamin na madini hulinda mwili dhidi ya magonjwa.

“Wananchi wetu lazima kujiepusha na kula vyakula bila kuzingatia aina na kiasi kulingana na mahitaji ya mwili. Ulaji huu huweza kusababisha kupungua au kuzidi kwa virutubishi mwilini,” aliseam afisa habari huyo.

Ulaji usiofaa ni pamoja na kula vyakula vyenye mafuta mengi hasa yale yatokanayo na wanyama, kula vyakula vyenye chumvi nyingi, sukari nyingi, kula chakula kupita kiasi, kukoboa nafaka na kutokula mbogamboga na matunda kiasi cha kutosha.

Mambo yanayoongeza uwezekano wa kupata magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni pamoja na ulaji usiofaa hasa matumizi ya chumvi kwa wingi, mafuta na sukari, uzito uliozidi, unene uliokithiri, kutofanya mazoezi, uvutaji wa sigara na bidhaa zitokanazo na tumbaku, unywaji pombe kupita kiasi na msongo wa mawazo.

Ili kuzuia ugonjwa wa kisukari na maradhi mengine yasiyo ya kuambukiza ni muhimu kufuata kanuni za afya ambazo ni ulaji bora, na mtindo bora wa maisha ambao ukifuatwa vyema huweza kwa kiasi kikubwa kuzuia mtu kupata kisukari au kwa mtu ambaye tayari ana ugonjwa wa kisukari hupunguza uwezekano wa kupata madhara makubwa ya kiafya.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...