Skip to main content

JESHI LA POLISI KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI MKOANI IRINGA CHA KUSANYA 1,218,960,000/-



Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akitoa hotuba yake jana wakati wa kufunga maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani, kulia kwake ni mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa Salim Abri Asas na katibu wake RTO Leopold Fungu. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA) 






JESHI la Polisi kikosi cha usalama barabarani mkoani Iringa kimefanyiwa kukusanya 1,218,960,000/- kutokana na makosa mbalimbali ya usalama barabarani katika kipindi cha miezi tisa mwaka 2016, imeelezwa. 

Katibu wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa ambaye pia ni mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa (RTO) Leopold Fungu alisema kuwa mapato hayo yameongezeka kwa asilimia 31 ikiliganisha na makusanyo ya mwaka 2015 kwa kipindi hicho hicho. 

RTO alisema kuwa mapato hayo yameongezeka hadi 1,218,960,000/- mwaka 2016 kutoka 835,800,000/- mwaka jana. 

Aidha, alisema kuwa makosa ya kawaida yameongezeka kutoka 27,787 mwaka 2015 hadi 40,632, ambapo ni sawa na aslimia 32. 

Kwa mujibu wa tathimini ya ajali za barabarani kwa kipindi cha miezi tisa mwaka 2015 ikilinganishwa na kipindi kama hicho cha mwaka huu 2016 mkoa wa Iringa umefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali za barabarani. 

Kuwa kwa kipindi cha January hadi Septemba mwaka 2015 ajali zilikuwa ni 41 ila kwa kipindi cha January 2016 hadi septemba 30 ni ajali 35 ndizo zilizotokea wakati watu waliopoteza maisha kwa kipindi cha January 2015 hadi Septemba ilikuwa ni 34 ila kwa mwaka huu toka January hadi Septemba 30 ni watu 30 ndio waliopoteza maisha. 

Aidha katika kipindi hicho ajali za piki piki zimepungua kwa asilimia 15 huku watu waliokufa kwa ajili ya pikipiki wamepungua kwa asilimia 11 na waliojeruhiwa wamepungua kwa asilimia 20 kuwa kupungua kwa matukio ya ajali ni kutokana na elimu za mara kwa mara. 

MKUU wa mkoa wa Iringa Amina Masenza ambaye alikuwa mgeni rasmi aliipongeza kamati ya usalama barabara mkoa wa Iringa chini ya mwenyekiti wa kamati hiyo Salim Abri Asas kwa kuokoa maisha ya watanzania kutokana na ajali. 

Masenza alitoa pongezi hizo jana (Jumamosi) wakati wa akifunga maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama ambayo imeadhimishwa kimkoa katika viwanja vya stendi ya mabasi yaendayo mikoani mjini Iringa. 

Mkuu huyo wa mkoa alisema mbali ya kuwepo kwa wadau mbali mbali katika kupunguza ajali na kusaidia pindi ajali zinapotokea ila serikali yake ngazi ya mkoa inatambua mchango mkubwa unaotolewa na familia ya mfanyabiashara Asas katika kusaidia kuokoa roho za watanzania pindi wanapopatwa ajali. 

“ Kana mambo mengi makubwa ambayo Asas amekuwa akijitolea kuyafanya kwa ajili ya kunusuru maisha ya majeruhi wanaopatwa na ajali ndani ya mkoa wetu, mfano katika ajali iliyotokea Changarawe mjini Mafinga kwa kuhusisha basi la Majinja ajali iliyoua watu zaidi ya 50 na kujeruhi wengine wengi …msaada mkubwa wa kuokoa roho za majeruhi kwa kujitolea dawa zilionyeshwa na Asas ….mimi nikiwa ni mkuu wa mkoa na serikali ya mkoa tunapongeza kazi nzuri ya Asas na familia yake katika kuokoa roho za majeruhi naomba Mwenyezi Mungu azidi kumuongezea pale anapopunguza kwa ajili ya wengine,” alisema mkuu wa mkoa huyo. 

Alisema kuwa wiki ya nenda kwa usalama ni kwa ajili ya kukumbushana mema yanayohusu kufuata sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuondoa vifo vinavyotokana na ajali barabarani hivyo pamoja na kumbushana kanuni na sheria za usalama barabarani ni vema kutumia maadhimisho hayo kutambua michango mbali mbali ya wadau wanaojitolea kwa jili ya kufanikisha elimu ya usalama bararani ama kusaidia kuokoa majeruhi na vinginevyo. 

“ Kumekuwepo na ongezeko kubwa la ajali za barabarani zinazohusisha pikipiki ajali hizi zinaweza kuepukika endapo waendesha na wapanda pikipiki watazingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ….natoa wito kwa wapanda pikipiki kuacha tabia ya kuendesha bila kupata mafunzo na kutokuwa na leseni suala la kuvaa kofia ngumu kwa madereva na abiria ni lazima …..acheni tabia ya kubeba abiria zaidi ya mmoja (mshikaki) …..pia kuacha kunywa pombe vikiwemo viroba wakati wa kutoa huduma ya usafiri …..kweli naumia sana kuona vijana wanakufa baada ya kuendesha pikipiki huku wakiwa wamelewa viroba”alisema mkuu huyo wa mkoa. 

Kwa watumiaji wengine wa barabara ni vema kuzingatia sheria za usalama barabarani kwa kufunga mikanda pindi wanapokuwa katika magari pia abiria kuacha kushabikia mwendokasi na badala yake kuwafichua madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani. 

Aidha alitaka kuanzia sasa dereva boda boda atakayebainika kusababisha ajali na kuita wenzake kwa ajili ya kumfanyia vurugu aliyesababishiwa ajali kukamatwa na washiriki wake na kufikishwa mahakamani. 

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa Salim Abri alisema kuwa kuna dhana potofu kwa baadhi ya watu kufikiri suala la usalama barabarani linahusu ajali pekee yake kwani hata kupiga honi bila sababu ama kukwamisha shughuli za barabara kwa mambo binafsi pia ni kero kwa watumiaji wengine wa barabara. 

“Tunapozungumzia sheria za usalama barabarani situ kwa ajili ya kuepusha ajali ila ni pamoja na kuepusha kero za usalama barabarani baadhi yetu tumekuwa tukifikiri usalama barabarani ni kuepusha ajali tu ila ukweli ukizingatia usalama barabarani ni pamoja na kero kubwa ya kutozingatia sheria za usalama barabarani hata kupiga honi bila sababu ni kero..., ” alisema Asasi. 

Alisema katika watumiaji wa vyombo vya moto wanaoongoza kwa kuvunja sheria za usalama barabrani na kero nyingine za barabarani ni boda boda hivyo angependa kuwaomba waendesha boda boda kupunguza kero za usalama barabarani zikiwemo za kupiga honi ovyo na ajali zinazoweza kuepukika . 




Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...