Skip to main content

NGONO ZEMBE YACHOCHEA UTOAJI MIMBA


Muuguzi Mwandamizi wa Zahanati ya Ugesa Theresia Augustino Chaula 


MUFINDI: Muuguzi Mwandamizi wa Zahanati ya Ugesa katika Kata ya Ihalimba wilayani Mufindi, mkoani Iringa Theresia Augustino Chaula wanawake wengi wanatoa mimba kiholela hali inayopelekea vifo kwa mabinti na wanawake waliopo kwenye ndoa.

Alisema kuwa tatizo la utoaji mimba katika kijiji cha Ugesa ni kubwa na wanakuja hospitali wakiwa na hali mbaya kiafya baada ya kutoa mimba mitaani.

“Wanawake wengi wanaofika hospitalini hapo wanadai mimba imetoka yenyewe wanaogopa kukosa huduma…,” alisema Chaula.

Chaula alisema jana wakati akiongea na Nipashe kuwa kuna baadhi ya wanawake hujaribu kutoa mimba kwa kuingiza vifaa vyenye ncha kali au vitu vichafu tumboni au kwa kujipiga makonde tumboni. 

Alisema kuwa mojawapo ya madhara makubwa ambayo yanampata mwanamke anayetoa mimba vichochoroni ni kutokwa na damu nyingi na kupasuka kwa kizazi.

Alisema kuwa vitendo hivi ni hatarishi na kamwe mwanamke yeyote asifanye hivyo, kwa kuwa vinaweza kusababisha majeraha yenye athari kubwa tumboni, ikiwa pamoja na kuvuja damu nyingi na hivyo kuleta kifo. 

Alisema wapo wanawake wanaotoa wasichana na wanawake mimba kwa kuingiza vifaa vyenye ncha kali au vitu vichafu tumboni.

Alisema kuwa Kijiji cha Ugesa kina tatizo la ngono zemba kutokana na ulevi wa pombe za kinyeji aina ya Ulanzi.

“Katika msimu huu wa pombe watu wamekuwa wakishiriki ngono zembe kunakopelekea mimba zisizotarajiwa na hatimaye kutoa mimba kiholela…,” alisema Chaula.

Alisema kuwa anakusudia kuitisha mkutano wa kijiji ili kuwabaini watu wanaotoa (maarufu kama ngariba) mimba mabinti na wanawake ili wachukuliwe hatua.

Wakati huohuo, muuguzi mwandamizi huyo, alisema zahanati hiyo inaupungufu wa watumishi wa afya ambapo aliongeza kuwa kwa pekee yake hataweza kulingana wingi wa wagonjwa wanaofika kwa matibabu.

Alisema kuwa ili huduma za afya ziendelee kwa ufanisi kunahitaji kuwepo na muuguzi mmoja, tabibu msaidizi mmoja na mhuduma mmoja.

Kijiji cha Ugesa ni moja ya vijiji ambavyo kwenye mradi wa kuendesha midhalo kuhusu migogoro ya ardhi inayotekelezwa na Shirika la TAGRODE kwa kushirikiana na shirika la PELUM Tanzania la mkoani Morogoro.

Shirika hilo linaendesha midahalo hiyo katika vijiji vya Ikuka, Mbigili, Mawala, Mawambala na Masalali kwa Wilaya ya kilolo.


Na katika vijiji vya Usokami, Ugesa, Makungu, Magunguli na Isaula Wilaya ya Mufindi kupitia mradi wake wa CEGO unaohusisha jamii ya vijijini katika uwajibikaji wa masuala ya ardhi ya kijiji.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...