Skip to main content

Padri Fred Njuguna: Elimu Ya Ufundi Stadi Inaweza Kutatua Tatizo La Ajira Nchini




Mmliki wa SIMBAYA BLOG Friday Simbaya (kulia) akimpongeza mmoja wa wahitimu Pelegrin Kilwa katika Mahafali ya 25 ya Chuo cha Wasalesiani wa Don Bosco mkoani Iringa hivi karibuni. 












VIJANA wameshauriwa kujiajiri kupitia elimu ya ufundi stadi ili kusaidia serikali kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira nchini.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Don Bosco (DYTC) cha mkoani Iringa, Padri Fred Njuguna wakati wa Mahafali ya 25 ya chuo hicho jana.

Chuo hicho kipo chini ya shirika la Waslesiani wa Don Bosco, ambalo ni shirika la kimataifa la kidini linalofanya kazi katika nchi 125 duniani kote kwa sababu ya vijana.

Padri Njuguna alitoa rai hiyo kwa vijana nchini wanaomaliza kidato cha nne na cha sita kwamba wanatakiwa kujiunga na vyuo hivyo vya elimu ya ufundi stadi baada ya kukosa kujiunga katika vyuo vya kawaida kutokana na sababu mbalimbali.

Alisema wapo wanafunzi wanaomaliza elimu hiyo ya sekondari ambao wanabweteka na kujikuta wanakaa bila kazi yakufanya, kumbe wangejiunga na vyuo hivyo vya ufundi stadi wangepunguza changamoto ya ukosefu wa ajira.

Alisema kuwa ili kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano ya sera ya viwanda, wahitimu hao wa elimu ya sekondari hawanabudi kujiunga na vyuo hivyo vya ufundi stadi.

Aidha, mkuu wa chuo hicho ameipongeza serikali kwa kuboresha mifumo ya utoaji mafunzo katika vyuo vya ufundi stadi nchini kunakopelekea wahitimu wengi katika vyuo hivyo kuajirika au kujiajiri wenyewe.

Alisema kuwa baada ya mamlaka ya vyuo vya elimu ya ufundi stadi nchini (VETA) kuboresha shughuli za mafunzo wahitimu wengi wamekuwa wakijiajiri wenyewe.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Chuo cha Ufundi cha Vijana cha Don Bosco Pd. Njuguna alisema kuwa chuo hicho kinakabiliwa na chamgamoto nyingi ikiwemo ya kukosekana kwa hosteli za wanafunzi ambapo wengi wao huishi mitaani na kusababisha utoaji wa malezi kwa vijana hao kuwa ngumu.

“Tunaweza kutoa malezi bora kwa vijana wanapokuwa shuleni lakini pindi wanaporudi nyumbani anaendelea na tabia zao zilezile, kumbe wangekuwa wanakaa hosteli inakuwa rahisi kutoa malezi kwa vijana…,” alisema Pd. Fred Njuguna.

Alisema kuwa changamoto nyingine ni kwamba chuo hicho kinatumia gharama kubwa ya kuendeshaji kwa kukosekana kwa ruzuku kutoka serikalini pamoja na wanafunzi wengi kushindwa kulipa ada kwa wakati.

Alisema kuwa kwa kawaida serikali inatakiwa kuchangia asilimia 70 ya uendeshaji wa vyuo vya ufundi stadi na asiliamia 30 inayobaki inachangiwa na chuo husika, “…lakini fedha hizo haziji mara nyingi,” aliongeza Pd. Njuguna.

Alisema pia kuwa changamoto nyingine ni kwamba kumekuwepo na idadi ndogo ya wanafunzi wa kike wanaoujiunga na chuo ukilinganisha na idadi yawavulana kutokana ukosefu wa hosteli.

Alitoa mfano kwa wahitimu wa mwaka huu, kwamba jumla ya wanafunzi 63 waliohitimu mwaka huu lakini ni wasichana nane tu ndio waliohitimu kutokana sababu mbalimbali ikiwemo mimba mbili za wanafunzi wa kike kwa kukosekana kwa mabweni ya shule.

Alisema kuwa chuo hicho kina zaidi ya wanafunzi 200, kati yao wasichana ni 47 kati ya wanafunzi wote wa chuo kutokana kutokuwa na mabweni.

Kituo cha mafunzo ya vijana cha Don Bosco kipo chini ya Wasalesiani wa Don Bosco ambalo ni shirika la kimataifa la kidini linalofanya kazi katika nchi 125 duniani kote kwa sababu ya vijana. 

Medrick msamila ni mhitimu katika mahafali ya 25 ya chuo hicho katika fani ya uashi amemshukuru mungu kwa kumaliza salama lakini akaweka msisitizo kuwa chuo hicho kione haja ya kupunguza ada ili wanafunzi wengi wajiunge na chuo.

Alisema kuwa wanafunzi wengi wanatoka kwenye familia zenye kipato kidogo lakini wanashindwa kujiunga kutokana na ada kubwa na kuongeza kuwa wasichana wengi wajiunge na vyuo vya ufundi stadi kwani ufundi sio tu kwa wanaume.

Wasalesiani wa don bosco waliwasili mkoani Iringa mwaka 1980 na walianzisha kituo cha vijana na shule ya kiufundi. 

Chuo hicho cha ufundi kinatoa jumla ya kozi za aina saba na kinasimamiwa na mamlaka ya elimu ya ufundi stadi nchini (VETA), ambapo asilimia 88 ya wahitimu wake wanajiajiri au kuajiriwa. 

Kozi zifuatazo zinatolewa katika Chuo cha Don Bosco Iringa ni pamoja na kozi ya kompyuta, uchapishaji, uchomeleaji, ushonaji, ufundi magari, umeme, na uashi.

Hata hivyo, mkuu wa chuo huyo amewashauri wahitimu kutoridhika na elimu walioipata na badala yake wajiendeleze mpaka wafike ngazi ya juu zaidi ili kuweza kuleta ubora na ufanisi katika kazi zao.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...