Skip to main content

RC AMINA MASENZA AZINDUA OPERESHENI KOMAZA





Na Esta Malibiche, Iringa


MKUU wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amezindua Operesheni Komaza,ambayo takribani Wanamgambo zaidi ya 200 wameshiriki katika zoezi la oparesheni komaza mkoani Iringa .


Mafunzo hayo yataenda sanjali na zoezi la kulenga shabaha ambalo litachukua siku nne porini likihusisha mazoezi ya ukakamavu pamoja na mazoezi mengine ya kijeshi kwa wanamgambo hao.


Akizungumza wakati wa kuzindua zoezi hilo lililofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Mlandege Manispaa ya Iringa Mkoani hapa likiwa limekusanya vijana toka vijiji vya Mboliboli, Wasa, Idodi na kwingineko wilayani Iringa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka viongozi wote wa siasa waache mara moja kuingilia shughuli yeyote inayohusishwa na jeshi la Mgambo,na kusema kuwa jeshi la mgambo kwani jeshi halina itikadi yoyote ya kichama
.
Masenza alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea vijana uwezo wa kuwa Imara kiafya, waweze kupambana pamoja na kuwaandaa kuwa vijana wazalendo katika jamii na kwa taifa kwa ujumla.


"Jeshi la mgambo lina msaada mkubwa sana katika ulinzi wa taifa hivyo ni muhimu sote tukachukulia mafunzo haya kama chachu ya maendeleo, ulinzi na usalama hivyo," alisema Masenza


Katika kuhakikisha zoezi linaenda sawa Mkuu wa Mkoa Amina Masenza alitoa gunia la mahindi ili likasaidie chakula kwa wanamgambo wakiwa mafunzoni na akatoa shukrani kwa wadau na kusema kuwa sasa kuna uhakikia kuwa vijana hawatapata shida kwenye suala la chakula.


Awali akimkaribisha Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela aliyataka makampuni ya ulinzi kuanza kutoa ajira kwa vijana waliopitia mgambo ili kupunguza idadi ya vijana wasio na ajira mtaani.


"Tumeamua kuwa na kikosi mahili ili kisaidie kupambana na majangili pamoja na wahamiaji haramu ambao wamekuwa tishio katika wilaya yetu," alisema RC.

Kwa upande wake mshauri wa mgambo wilaya ya Iringa Afande J.M Kita amewashukuru baadhi wa wadau kwa misaada waliyotoa katika kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa. 


Kita aliwataja baadhi ya wadau waliochangia kuwa ni pamoja na ndugu Salim Asas aliyetoa shilingi milioni moja ambayo imeziingizwa moja kwa moja katika kughalamia chakula kwaajili ya vijana hao, naye meneja wa TANROAD wilaya ya Iringa ametoa Mchele kwaajili ya vijana hao. Kisha Afande KITA akatoa rai kwa wadau ambao wataguswa kusaidia maana bado kuna uhitaji wa msaada wa hali na maali ili kufanikisha ziezi hilo.












Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...