Skip to main content

TAGRODE: MIGOGORO YA ARDHI KILOLO INATOKANA UGOMVI WA MIPAKA












Mkazi wa Kijiji cha Mawambala wilayani Kilolo, mkoani Iringa, Mzee Dominikus Mgogosi akitoa maoni wakati wa mdahalo wa nini kifanyke kumalizi migogoro ya ardhi ulioandaliwa shirika la TAGRODE chini ya mwavuli wa mashirika (PELUM Tanzania) kupitia ufadhili wa watu wa Marekani jana. (Picha: Friday Simbaya)




Na Friday Simbaya, Kilolo



MRATIBU wa shirika lisilo la kiserikali la TAGRODE yenye makao yake makuu mjini Iringa, Dickson Mwalubandu amesema migogoro yote ya ardhi wilayani Kilolo mkoani Iringa inatokana na ugomvi wa mipaka katika maeneo ya vijijini.



Alisema alishauri kuwa ni lazima mipaka ya vijiji ihakikiwe upya ili kupunguza migogoro ya ardhi na mipaka inayovikumba baadhi ya vijiji wilayani Kilolo.



Mwalubandu alisema hayo jana (Ijumaa) wakati akiwasilisha mada katika mdahalo uliofanyika katika kijiji cha Mawambala wilayani humo ukilenga kutafuta mambo yakufanya ili kupunguza malalamiko ya migogoro ya ardhi. 



“Katika kuhakikisha wananchi wanakabiliana na changamoto hiyo shirika lake linaendesha midahalo na kuimarisha kamati za ardhi za vijiji na mabaraza ya ardhi ya vijiji ili yaweze kutatua migogoro pindi inapojitokeza kwenye maeneo yao,” alisema mratibu huyo.



Alisema midahalo hiyo inalenga kuwaongezea wananchi wa wilaya hiyo, hasa vijiji vya mradi uelewa juu ya sheria za ardhi, haki za ardhi kwa wanawake na makundi maalum pamoja na utatuzi wa migogoro ya ardhi.



Alisema kuwa kwa ufadhili wa shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani (USAID), kupitia mtandao wa Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali yanayofanya kazi na wakulima na wafugaji wadogo nchini Tanzania (PELUM Tanzania) shirika hilo linaendesha midahalo hiyo katika vijiji vya Ikuka,



Mbigili, Mawala, Mawambala na Masalali kwa wilaya ya kilolo na vijiji vya Usokami, Ugesa, Makungu, Magunguli na Isaula wilaya ya Mufindi kupitia mradi wake wa CEGO unaohusisha jamii ya vijijini katika uwajibikaji wa masuala ya ardhi ya kijiji.



akichangia mada, mkazi wa Kijiji cha mawambala alisema migogoro ya ardhi katika maeneo yao itakoma kama serikali itatakiwa kuhakiki mipaka ya vijiji,hatua ambayo pia itaimarisha amani na utulivu na kuifanya sekta hiyo kuwa na tija kwa jamii.



Kwa upande wake, Mzee Dominikus Mgogosi alisema serikali za vijiji ni chanzo cha migogoro kwa sababu zina baadhi ya viongozi wanaoshindwa kusimamia sheria hizo baada ya maamuzi kufanywa.



Kwa upande wake Expedito Lusoko ambaye ni mwenyekiti wa Kijiji cha Mawambala aliomba serikali kwa kutumia sheria hizo kutenga maeneo kwa ajili ya wakulima na wafugaji hatua itakayosaidia kuepukana na migogoro kwa kuwa makundi yote mawili yanategemeana.



Ushiriki wa Wananchi katika kusimamaia sekta ya Kilimo yaani Citizens Engaging in Government Oversight in Agriculture (CEGO-Agriculture) ni mradi wa miaka minne unaofadhiliwa na USAID na kutekelezwa na PELUM Tanzania. 



Mradi una lengo la kuongeza maarifa, kujenga ushahidi, na kuongeza uelewa wenye nia ya kuimarisha haki za ardhi kwa wakulima wadogo kwa maendeleo ya kiuchumi, maisha bora, na kilimo endelevu ili kuboresha utawala bora na uwajibikaji. Mradi unatekelezwa katika mikoa ya Morogoro, Iringa, na Dodoma.



PELUM Tanzania inatekeleza mradi wa kuhusisha jamii ya vijijini katika uwajibikaji wa masuala ya ardhi ya kijiji. Mradi huo unajulikana kwa jina la CEGO na unatekelezwa kwa ufadhili kutoka kwa watu wa Marekani.











Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...