Skip to main content

Tigo, Ebony FM kushirikiana uzinduzi tamasha la Mtikisiko mikoa ya Kusini




Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini, Jackson Kiswaga (kushoto) akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) juu ya uzinduzi wa matamasha ya Mtikisiko yanayolenga kunyanyua sekta ya muziki yatakayofanyika katika mikoa katika mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya kwa uratibu wa radio ya Ebony FM






Iringa: Kampuni inaongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali Tigo Tanzania leo imesaini rasmi uzinduzi wa tamasha la mwaka la Mtikisiko kwa kushirikiana na kituo cha redio cha Ebony FM ambacho kina wasikilizaji wengi katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Mtiririko wa matamasha hayo ya mwaka unatarajiwa kuanza Novemba 19 hadi 26 katika mikoa ya Njombe na Mbeya kwa pamoja ambapo onesho la fainali litafanyika Desemba 10, 2016 mkoani Iringa.


Akizungumza katika uzinduzi wa tamasha hilo mkoani Iringa, Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Kusini Jackson Kiswaga alisema, “Tigo kila mara inakuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba vipaji vinavyoibukia katika sekta ya muziki vinapewa jukwaa la kuonesha vipaji vyao na wasanii maarufu wanaweza kuunganishwa na mashabiki wao.


Tamasha la Mtikisiko linakuja baada ya kumalizika kwa Tamasha la Tigo Fiesta 2016 hivi karibuni ambalo Tigo ilikuwa mdhamini mkuu. Kiswaga aliwaaambia waandishi wa habari kwamba mashabiki watarajie ubora ule ule wa burudani waliouzoea wakati wa tamasha la Fiesta.


Kushiriki kwa Tigo kutakwenda sambamba na kuhakikisha wateja wa Tigo na wale ambao sio wateja wanafahamu na kuzielewa huduma za Tigo wakati wa tamasha.


“Katika kukuza uzoefu wa mteja na mtumiaji wakati wa tamasha, tunatarajia wateja wetu kutumia vilivyo kuanzishwa kwa huduma ya 4G LTE, Tiogo Pesa na bidhaa na huduma nyingine zinazotolewa,” alisema Kiswaga.


Kiswaga alitangaza kuwa washiriki wa tamasha hilo kwa mwaka huu watakuwa na nafasi ya kuchagua njia ya kupata tiketi zao kupitia Tigo Pesa bila gharama ya ziada.


Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo washiriki wote wa tamasha ambao watanunua tiketi zao kupitia Tigo Pesa watafurahia faida kwa kupata [punguzo la asilimia kumi kwa kila tiketi itakayonunuliwa


Kiswaga alifafanua, “Kununua tiketi kupitia Tigo Pesa, wateja kutoka mtandao wowote watapiga namba ya Mfumo wa Kifedha wa Simu (mfano *150*01# kwa Tigo), halafu chagua, “tuma pesa”, ikifuatiwa na chagua, “Mitandao Mingine” halafu chagua, “Tigo Pesa” na mwisho ingiza namba 0674444444. 


Kwa upande wake mratibu wa Tamasha la Mtikisiko 2016, Austine Nyondo alisema, “Ninapenda kuchukua nafasi hii kuwaashukuru Tigo wakiwa ni wadhamini wakuu wa tamasha hili; mashabiki wetuwatarajie kupata burudani kutoka kwa wasanii maarufu katika sekta ya muziki.”


Aliarifu kuwa wakati wa tukio hilo watasambaza vipeperushi kwa vijana ambavyo vitakuwa na ujumbe unaohusu Virusi Vya Ukimwi (VVU) kutokana na sababu kwamba mikoa ya kusini inachukuliwa kuwa ni “ukanda ulioathiriwa” na janga hilo.


Tamasha maarufu la Mtikisiko ambalo awali lilijulikana “Together Time” lilibadilishwa jina mwaka 2008 lilianza mwaka 2007 na limeendelea kukua katika kipindi chote cha miaka hiyo na kupata umaarufu kama tamasha la burudani la mwisho wa mwaka katika mikoa ya kusini.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...