Skip to main content

BODI YA FILAMU NCHINI YAWATAKA WADAU KUFIKISHA MISWADA YA FILAMU KUKAGULIWA KABLA YA KUIGIZWA



Bi.Deograsia Ndunguru ambaye ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Sanaa na Habari, Chuo Kikuu Dodoma UDOM, hii leo akiwasilisha mada kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara, yaliyoanza jana ukumbi wa shule ya Sekondari Mara. Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Bodi ya Filamu nchini. 




Mtendaji Mkuu Taasisi ya Sanaa Bagamoyo, Dkt.Herbert Makoye, hi leo akiwasilisha mada kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara, yaliyoanza jana ukumbi wa shule ya Sekondari Mara. 


Wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara wakifuatilia mada kutoka kwa Mtendaji Mkuu Taasisi ya Sanaa Bagamoyo, Dkt.Herbert Makoye. 


Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fissoo (kushoto), akizungumza wakati wa mafunzo hayo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo jana. Baada ya ufunguzi alishiriki na wadau wengine mafunzo hayo. 


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, akizungumza kwenye mafunzo kwa wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara, hii leo. Kutoka kushoto ni Mtendaji Mkuu Taasisi ya Sanaa Bagamoyo, Dkt.Herbert Makoye, Bi.Deograsia Ndunguru ambaye ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Sanaa na Habari, Chuo Kikuu Dodoma UDOM na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fissoo 


Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba (kuhoto) akiwa pamoja na Afisa Utamaduni Halmashauri ya Musoma Vijijini, Twalib Kamugisha (kulia) wakifuatilia mafunzo kwa wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara. 


Afisa Utamaduni Halmashauri ya Musoma Vijijini, Twalib Kamugisha (kushoto) akiwa pamoja na Katibu wa Chama cha Waigizaji mkoani Mara TDFAA, Johnson Ibambai maarufu kama Dunia (kulia), wakifuatilia mafunzo kwa wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara 


Wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara, wakiwa kwenye mafunzo ya filamu yanayotolewa na Bodi ya Filamu mkoani humo. 



Bodi ya Filamu nchini imewataka wadau wa sekta hiyo kuwasilisha miswada ya kazi zao ili kukaguliwa kabla ya kuanza kuigiza ili kuondona na usumbufu wa kuzifungia kazi zisizo na maadili. 






Katibu Mtendaji wa bodi hiyo, Joyce Fissoo, ametoa kauli hiyo kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia ya filamu mkoani Mara, yanayofanyika Mjini Musoma. 


Amesema hatua hiyo itasaidia kuondoa usumbufu wa ambao umekuwa ukijitokeza kwa baadhi ya miswada ya filamu kurekodiwa kabla ya kukaguliwa na baadaye filamu zake kuzuiliwa wakati wa kuingia sokoni hivyo kuibua usumbufu mkubwa. 


Wakiwasilisha mada kwenye mafunzo hayo, Dkt.Herbert Makoye kutoka Taasisi ya Sanaa Bagamoyo pamoja na Deograsia Ndunguru kutoka Chuo Kikuu Dodoma, wamewahimiza wanatasnia wa filamu kuzingatia weledi katika uandaaji wa kazi zao kwa kuzingatia maudhui bora pamoja na maandalizi yanayokidhi uhitaji. 


Washiriki wa mafunzo hayo wameelezea umuhimu wake ambapo wamesema yatawasaidia kuboresha uzalishaji wa kazi zao ikiwemo kuzingatia maudhui bora tofauti na ilivyokuwa hapo awali. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...