Skip to main content

JESHI LA POLISI MKOANI IRINGA LAJIPANGA KUKARIBILIANA NA VITENDO VYA UHALIFU

Image result for RPC IRINGA JULIUS MJENGIImage result for RPC IRINGA JULIUS MJENGI

Jeshi la Polisi mkoani Iringa lasema limejipanga kukabiliana vitendo vyote vya uhalifu kuelekea katika kipindi cha sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya na kuonya kuwa kamwe watu wasidhubutu kufanya fujo.

Akiongea na SIMBAYABLOG leo  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Kamshina Msaidizi wa Polisi (ACP), Julius Mjengi alisema kuwa jeshi la polisi limejipanga kukabiliana na vitendo vyote vya kihalifu.

Alisema kuwa katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya, Jeshi la Polisi linatoa tahadhari kwa wananchi wote kuwa makini na kuchukua hatua stahiki na za haraka kwa kutoa taarifa pindi wanapoona viashiria vyovyote vya uhalifu katika maeneo wanamoishi na sehemu mbalimbali zikiwemo maeneo ya biashara na nyumba za ibada.

Ikumbukwe kuwa, wananchi wenye imani ya kikristo hutumia muda huo kwenda kuabudu siku ambayo wanakumbuka kuzaliwa Yesu Kristo pamoja na mwendelezo wa sherehe hizo kwenye maeneo mbalimbali ya starehe. 

Uzoefu unaonyesha kuwa baadhi ya watu hutumia kipindi hicho cha sikukuu kama mwanya wa kufanya matukio ya uhalifu kutokana na mikusanyiko hiyo ya watu. 

Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha kwamba, wananchi wote wanasherekea sikukuu hizo kwa amani na utulivu, pasipo vitendo ama viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani, alisema kamanda huyo.

Alisema kuwa Jeshi la Polisi litamarisha doria maeneo yote hapa mkoani pamoja na kufuatilia mienendo na kukamata watu wote wataochochea, kuhamasisha na kushiriki katika vitendo vya uhalifu, vurugu na fujo.

“Tukiwa katika kipindi hiki cha kusherehekea Krismasi na Mwaka Mpya, nawaomba wananchi mkoani hapa kushirikiana na jeshi la polisi kuhakikisha ulinzi na usalama mkoani hapa vinaimarishwa na wale wote watakayebainika kufanya uhalifu wanakamatwa na sheria ichukua mkondo wake,” alisema kamanda Mjengi.

Alisema kuwa jeshi la polisi pia itaimarasha usalama katika nyumba zote za ibada na kuwaomba waumini kutoa ushirikiana kwa jeshi hilo.

Katika hatua nyingine, jeshi la polisi limepiga marufuku vitendo vya kuchoma matairi, kukimbizi magari huku madereva wakiwa wamelewa pamoja na kupiga mafataki.

Jeshi hilo limesema kuwa litahakikisha watu wanasherehekea siku hizo mbili za krismasi na mwaka mpya kwa amani na utulivu.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...