Skip to main content

KIPONZELO FC YAICHAPA TIMU YA MAKONGATI 3-0 KATIKA KOMBE LA J. MSOFU









Mdhamini wa mashindano ya Kombe la J. Msofu, Jeremia Edward Msofu (wa pili kulia) akikabidhi vifaa vya michezo kwa mmoja ya timu zinazoshiriki mashindano hayo katika Kijiji cha Kiponzelo Kata ya Kiponzelo, Jimbo la Kalenga wilaya Iringa, mkoani Iringa jana, (Picha na Friday Simbaya)






Timu ya Soka ya Kiponzelo ya Kijiji cha Kiponzelo, Kata ya Maboga, Jimbo la Kalenga wilayani Iringa imeibuka mshindi dhidi ya wapinzani wake Timu ya Soka ya Makongati ya Kijiji hicho kwa kuilaza magoli 3-0 kwenye pambano la ufunguzi ya Kombe la J.Msofu lililopigwa katika Uwanja wa michezo wa Shule ya Sekondari Kiponzelo jana.

Mashindano ya Kombe hilo lililoandaliwa na Jeremia Edward Msofu ambaye pia ni mmliki wa kampuni ya mabasi ya ‘OTA HIGH CLASS’ kwa kushirikiana na chama cha mpira wilayani Iringa lilioanza rasmi tarehe 11 Desemba 2016.

Timu ya Soka ya Kiponzelo wenyeji waliovalia jezi ya rangi nyeusi walijipatia goli la kwanza kupitia mshambuliaji wao machachali Efeso Makaye (9) ambaye ndiye alikuwa nahodha wa timu hiyo dakika 44 katika kipindi cha kwanza.

Hadi mapumziko timu ya kiponzelo ilikuwa inaongoza kwa goli moja lakini kipindi cha pili kilipoanza timu zote zilishambuliana na kupelekea timu ya kiponzelo kupata goli la pili kupitia mshambuliaji wake aliyefunga bao la kwanza dakika chache kwa kuanza kipindi cha pili.

Wakati timu ya soka ya Makongati ya kijiji cha Makongati waliovalia jezi ya rangi ya zambarau, Kata ya Maboga haijakaa sawa waliongezwa goli la tatu wakati huo kupitia uwinga wa kulia wa timu ya kiponzelo Yesus Mamba.

Mechi ya ufunguzi hiyo ya Kombe la J. Msofu ilichezeshwa na mwamuzi Ahmad Mzee akisaidiana na wasaisizi wake steven Makuka na Daud Mgimba.

Kwa upande wake, mdhamini wa mashindano hayo Jeremia Msofu alisema kuwa lengo la mashidano hayo nikuibua vipaji vitakavyoweza kuunda timu ya Jimbo la Kalenga itakayoweza kucheza kuanzia ligi ya daraja la nne la hadi ligi kuu Tanzania (VPL).

Alisema kuwa mashindano hayo hayana mlengo wa kisiasa, bali ni kuibua vipaji na isitoshe yeye ni mzaliwa wa Kijiji cha Kiponzelo Kata ya Maboga katika Jimbo la Kalenga wilayani Iringa,mkoani Iringa.

“Kwa kuanzia nimeamua kuanza na kata mbili ambazo zinajumlisha vijiji vinane lakini hapo baadaye nakusudia kufanya kwa Jimbo la Kalenga lote Mungu akipenda…” alifafanua Msofu.

Msofu alitoa vifaa vya michezo kwa kila timu shiriki kwa kupewa jezi seti moja na mpira moja kwa kila kijiji kushiriki.

Naye mratibu wa mashindano hayo Abuu Changawa ‘Majeki’, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Lipuli FC ya mjini Iringa aliwasisitizia wachezaji wanaoshiriki Kombe la Jeremia (J.MSOFU CUP 2016) kuzingatia nidhamu.

Aidha, mratibu huyo alisema kuwa jumla ya vijiji nane kutoka kata ya maboga na Wasa, ambavyo ni Wasa, Usengelindete, Ufyambe na Ikungwe, (kata ya Wasa), Kiponzelo, makongati, Magunga na Itengulinyi vya kata ya Kiponzelo vinashiriki katika kombe hilo.

Kwa upande wa zawadi mratibu huyo alisema kuwa mshindi wa kwanza atapa ng’ombe mmoja, mshindi wa pili mbuzi wawili na mshindi wa tatu atapata mbuzi mmoja na kuongeza kuwa gharama ya mashindano hayo ni zaidi ya shilingi milioni kumi.

Mashindano hayo yalizinduliwa rasmi na Katibu wa Chama cha Mpira Iringa Vijijini ,Juma Lalika, ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya uchaguzi wa Chama cha Mpira Tanzania (TFF)







Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...