Skip to main content

MAZISHI YA KIHISTORI IRINGA MAREHEMU AZIKWA KABURI MOJA NA KONDOO


Wanafamilia wakiwa wamelizungika kaburi la marehemu Ngaga aliyezikwa kaburi moja na kondoo pamoja na kuku mweusi leo kwenye kitongoji cha Mkawaganga kijiji cha Mbigili wilaya ya Kilolo mkoani Iringa 

Mganga wa kienyeji Galasiano Nyenza (kulia) akiwa na mtoto wa marehemu Andrea Ngaga ,Kurugenzi Ngaga kushoto baada ya kufanyika kwa mazishi ya kimila katika kijiji cha Mbigili Kilolo kwa marehemu kuzikwa kaburi moja na kondoo na kuku mweusi 

Mganga Nyenza aliyeongoza mazishi hayo katikati akiwa na baadhi ya ndugu kando ya kaburi 

Waombolezaji wakitoka kuzika 

 
 Marehemu enzi za uhai wake 

Nyumbani kwa marehemu waombolezaji wakiwa kwenye foleni 
....................................................................................................
Na MatukiodaimaBlog
MAMIA ya wakazi wa kijiji cha Mbigili na mji wa Ilula katika wilaya ya Kilolo wamefurika katika mazishi ya aina yake yaliyofanyika katika kitongoji cha Mkawaganga kijiji cha Mbigili wilaya ya kilolo mkoani Iringa kushuhudia mazishi hayo ya kihistoria baada ya mzee mmoja aliyefariki dunia ghafla kuzikwa kaburi moja na kondoo pamoja na kuku mweusi.


Tukio hilo limetokea leo wakati wa mazishi ya mzee Andrea Ngaga (90) mkazi wa kitongoji cha Mkawaganga aliyekuwa akijishughulisha na kazi za uganga wa kienyeji kijijini hapo enzi za uhai wake .


Baadhi ya wananchi waliofika katika mazishi hayo walisema kuwa walilazimika kusitisha shughuli zao za shamba na biashara na kufika kushuhudia mazishi hayo ambayo ni mara ya kwanza kufanyika katika kijiji hicho alisema John Mfaligoha kuwa kabla ya kifo marehemu huyo alipata kuwaeleza aina ya mazishi yake yatakavyokuwa .


Hivyo alisema wananchi waliowengi walifika kutaka kushuhudia tukio hilo la mazishi na ndio sababu iliyopelekea wananchi kusukumana msibani wakati wa mazishi kwa kila mmoja kutaka kushuhudia tukio hilo la kihistoria katika kijiji hicho.


Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Mbigili Ibrahim Rashid (46) alisema amezaliwa katika kijiji hicho tukio hilo ni la kwanza kufanyika hajapata kushuhudia mazishi ya aina hiyo zaidi ya kusikia katika vyombo vya habari kutoka nje ya kijiji chake na kuwa mazishi hayo yamefanyika kimila zaidi na kimsingi huwa marehemu anachagua mtu wa kuzikwa nae kabla ya kifo .


Ila hakuweza kuacha maagizo zaidi ya kuomba pindi atakapokufa kuzikwa kimila na ndio sababu aliyeongoza mazishi hayo ni mganga wa kienyeji kutoka Ifunda wilaya ya Iringa Galasiano Mfaume Nyeza ambae ni baba mdogo na marehemu huyo .




Mtendaji wa serikali ya kijij hicho cha Mbigili Thabith Kalolo alisema kuwa kimsingi hakuna kosa lolote familia ambalo wamelifanya kwa kufanya mazishi ya aina hiyo kwani serikali haiingilii uhuru wa wananchi wake kuamini masuala ya mila na kuwa iwapo mazishi hayo yangekiuka haki za binadamu mwingine mfano kama wangekata kumzika marehemu na binadamu mwingine aliyehai hapa isingewezekana ila kwa kumzika na kondoo na kuku mweusi hakuna shida .


Hata hivyo alisema tofauti ya rekodi ya misiba iliyopata kutokea katika kijiji hicho ,msiba wa mganga huyo umevunja rekodi kwa kuhudhuriwa na idadi kubwa ya watu na kuwa msiba uliovunja rekodi kwa michango ni huo pekee kwani misiba mingine fedha za rambi rambi huwa ni kati ya Tsh 300000 hadi 500000 mwisho ila msiba huo rambi rambi ni zaidi ya Tsh milioni 1.3


Mtoto wa marehemu Kurugenzi Ngaga alisema kuwa babake alifariki dunia juzi Desemba 20 majira ya saa 6 usiku mwakla huu kuwa alikuwa akisumbuliwa na tatizo ya chembe ya Moyo na kuwa ameacha wajane wawili na watoto 19.


Kurugenzi alisema kimila kama ingekuwa zamani marehemu angezikwa na mjukuu wake aliyemteua kushika mikoba yake ila kutokana na mambo ya mila kwa sasa kupewa kisogo waliona ni vema wakamzika na kondoo na kuku huyu mweusi .

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...