Skip to main content

MEYA DAR ES SALAAM AWAONYA WAKUSANYA USHURU WA MAEGESHO


Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akifafanua jambo kwa wandishi wa habari leo kuhusiana na suala zima la tozo za maegesho ya magari



MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amewataka wakandarasi hususani wanaokusanya ushuru wa maegesho, waanze kutumia mashine za EFDs walizokabidhiwa vinginevyo mikataba yao iko hatarini kusitishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Meya Mwita amesema kwa muda mrefu wakandarasi hao walikuwa wakitumia mashine za mkono, wamebaini mapato mengi yalikuwa yakipotelea mifukoni mwa watu wachache na sasa ni agizo kwa wazabuni wote wa wilaya za Daresalaam kutumia mashine za Kielectroni.

Amesema kupitia mashine hizo wanahakika mapato yataongezeka kutoka shilingi milioni 170 iliyokuwa inakusanywa hapo awali kwa mwezi hadi kufikia Zaidi ya Shilingi Milioni 370 kwa mwezi.

Katika hatua Nyingine, Isaya Mwita amewaonya wakandarasi hao kuangalia namna ya kuwadhibiti wafanyakazi wao kwani hivi sasa wamezusha tabia ya kuwanyanyasa wakazi wa Jiji la Darsalaam kinyume cha makubaliano ya mkaba.

Amesema kumekuwa na tabia za wakandarasi isivyo halali wakazi wa jiji wanaoegesha magari yao,pamoja na kutumia lugha za matusi kwa kisingizio cha kufuata sheria za Jiji.


Amesema sheria ya Jiji hairuhusu matumizi ya mabavu, matusi, kejeli kwa watu wanaoegesha gari zao, wanachopaswa kufanya ni kufuata sharia ambazo wamekubaliana katika mikataba yao ya kazi.


Meya ameyataja majukumu ya kimkataba ambayo wakandarasi wote wanapaswa kufuata ni kama ifuatavyo,:
1 .Wakala atafanya kazi hii bila Kuvizia magari ya wananchi kwa lengo la kujipatia pesa .


2. Wakala atafanya kazi hii kwa weledi mkubwa kwa kuzingatia Sheria, Miongozi, Maelekezo, Kanuni na taratibu zilizopangiwa pasipo kusababisha bughuza ,kero na usumbufu kwa Wananchi.


3. Wakala anatakiwa kutoa muda wa dakika sitini [60] kabla ya kuchukua mamuzi ya vuta gari, Bodaboda au bajaji lililovunja sheria, kuzuia . Lakini kwa gari , Bajaji au Bodaboda iliyozuia barabara itaondolewa mara moja ili kuondoa msongamano.


4.Wakala anapaswa kuepuka kutoa Lugha ya Matusi au udhalilishaji .


4.Wakala anapaswa kuruhusu gari ,Pikipiki au Bajaji kuegeshwa kwa dharura sehemu isiyoruhusiwa kwa muda usiozidi dakika Thelasini [30] kama Dereva ameweka viashiria vya tahadhari. Isipokuwa kwa wale wenye magari yenye hitilafu inaweza kuzidi mpaka saa moja [yaani dakika 60] baada ya kujirizisha na dharura iliyojitokeza.


5. Wafanyakazi wanapaswa kuwa na sare pamoja na vitambulisho vya kazi .


6. Wakala anatakiwa kutoa faini zilizoainishwa na jiji na sio vinginevyo.


7. Wakala anapaswa kutumia risiti za mashine za Kielekronikia.


8.Magari yanayotumika katika utekelezaji wa kazi hii yanatakiwa yawe na Stika kubwa inayoonyesha jina la kampuni pamoja na namba ya simu ya wakala.


9.Wakala anatakiwa kutumia risiti [Point of Sale, [POS] za Halmashauri ya jiji.




10. Wakala anatatakiwa kutoa taarifa ya utekelezaji wa kazi hii kwa MWAJIRI Kila baada ya Wiki Mbili.
11.Wakala anatakiwa kufanya kazi katika maeneo aliyoelekezwa na MWAJIRI nasio vinginevyo.


12. Wakala anapaswa kushirikiana na jeshi la polisi pamoja na Mamlaka zingine pale inapohitajika katika utekelezaji wa kazi husika.


Sasa anashangazwa kuona mikataba hiyo inavunjwa, amesema hatosita kufuta zabuni zote kwa kitendo cha kukiuka makubaliano hayo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...