Skip to main content

MMILIKI WA JAMIIFORUM AENDELEA KUSOTA LUMANDE



Mwanzilishi na Mtendaji Mkuu wa Mtandao wa JamiiForums, Maxence Melo akiongozwa na Askari Polisi wakati alipofikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jijini Dar es salaam leo, kusomewa mashtaka yanayomkabili kama inavyosomeka hapa chini.



Mwanzilishi-mwenza na Mkurugenzi wa Kampuni ya Jamii Media, Maxence MeloMubyazi (40), leo amepelekwa mahabusu baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana katika kesi moja kati ya tatu zinazomkabili ikiwamo ya kuzuia Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi na kuendesha mtandao wa Jamii Forum bila usajili.

Mapema leo asubuhi mshtakiwa huyo ambaye pia ni
mfanyabiashara na bosi wa mtandao huo, alifikishwa katika viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam mapema asubuhi.


Alipandishwa kizimbani saa 3:29 kusomewa mashtaka katika kesi yake ya kwanza mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Upande wa mashtaka uliongozwa na Wakili wa Serikali
Mwandamizi, Mohamed Salum akisaidiana na Wakili wa Serikali Mkuu, Yohanes Kalungula.

Wakili Salum alidai kuwa katika tarehe tofauti kati ya Aprili Mosi na Desemba 13, mwaka huu eneo la Mikocheni, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa akiwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Jamii Media Ltd, inayoendesha mtandao wa kijamii wa Jamiiforums, akiwa anajua polisi wanafanya uchunguzi kutokana na taarifa zilizochapishwa katika mtandao huo, alishindwa kutoa taarifa. Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alishindwa kutoa taarifa ambazo ziko chini yake huku akijua ni kosa.

Mshtakiwa alikana shtaka hilo, upande wa Jamhuri ulidaia kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika, na haukuwa na pingamizi la dhamana hivyo uliomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Hakimu Simba alisema mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa kuwa na wadhamini wawili wanaotoka taasisi zinazotambulika au serikalini, watakaotia saini hati ya dhamana ya Sh. Milioni 10 kila mmoja.

Mshtakiwa alitimiza masharti hayo dhidi ya kesi hiyo na imepangwa kutajwa Desemba 29, mwaka huu.

Katika kesi ya pili, mshtakiwa alisomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa. Wakili Salum alidai kuwa katika tarehe tofauti kati ya Mei 10 na Desemba 13, mwaka huu eneo la Mikocheni, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa kama Mkurugenzi wa Kampuni ya Jamii Media Ltd, inayoendesha mtandao wa kijamii wa Jamiiforums, huku akijua kwamba polisi wanafanya uchunguzi kuhusu taarifa zilizochapishwa katika mtandao wake, alishindwa kutoa taarifa hizo ambazo ziko chini yake. Mshakiwa alikana shtaka
hilo.

Upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado
unaendelea na haukuwa na pingamizi la dhamana na uliomba tarehe ya kutajwa. Hata hivyo, mshtakiwa katika kesi hii alishindwa kutimiza masharti ya dhamana kwa kutokuwa na wadhamini na alirudishwa mahabusu hadi Desemba 29, mwaka huu kesi yake itakapotajwa.

Katika kesi ya tatu, mkurugenzi huyo alipandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Wakili Salum alidai kuwa katika tarehe tofauti, kati ya Desemba,mwaka 2011 na Desemba 13, mwaka huu eneo la Mikocheni, jijini Dar es Salaam,mshtakiwa akiwa kama mkurugenzi wa kampuni hiyo, aliendesha mtandao wa kijamii
ujulikanao kama Jamiiforums.com bila kuwa na usajili wa kuendesha mtandao huo.

Katika shtaka la pili, katika tarehe tofauti, kati ya Januari 26
na Desemba 13, mwaka huu eneo la Mikocheni, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa akiwa mkurugenzi wa kampuni hiyo inayoendesha mtandao wa kijamii wa Jamiiforums huku akijua kwamba polisi wanafanya uchunguzi kuhusu taarifa zilizochapishwa katika mtandao wake alishindwa kutoa taarifa hizo ambazo ziko chini yake.

Mshtakiwa alikana mashtaka hayo. Upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Hakimu alisema mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa kuwa na mashahidi wawili wanaotoka taasisi zinazotambulika watakaosaini hati ya dhamana ya Sh. Milioni Moja kila mmoja pamoja na mshtakiwa. Mshtakiwa alitimiza masharti hayo na kesi yake itatajwa Januari 16, mwaka 2017.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...