Skip to main content

NYAMA YA NG'OMBE MJINI IRINGA YAPANDA SIKUKUU YA KRISMASI



Baadhi ya wateja wakiwa katika mmoja ya mabucha ya nyama ya ng’ombe leo mjini Iringa, mkoani Iringa wakati huu wa kusherehekea siku kuu ya Noeli. (Picha na Friday Simbaya)










IRINGA: Wakristo duniani kote wanasherehekea Sikukuu ya Krismasi, jana msongamano katika soko la Manispaa ya Iringa na mitaa maarufu ya Mashine tatu na Miyomboni iliongezeka, huku baadhi ya bidhaa zinazotumika kwenye sikukuu, ikiwemo nyama, zikiwa zimepanda bei.

Wakazi wa mjini Iringa wamesema bei ya nyama ya ng’ombe imepanda katika kipindi hiki cha sikukuu ya Krismasi.

Walisema kuwa nyama ya ng’ombe imepanda kutoka shilingi elfi sita hadi kufikia shilingi elfu sita na mia tano kwa kilo moja.

SIMBAYABLOG ilIshuhudia baadhi ya mabucha ya nyama ya ng’ombe yakiwa yamefurika wateja katika maeneo mbalimbali ya halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo asubuhi.

Elizabeth Kadaga ni mkazi wa Frelimo, Manispaa ya Iringa alisema kuwa wafanyabiashara huwa wanatumia mwanya wa siku kuu kama krismasi na mwaka mpya kuvuna faida kubwa kwa kupandisha bei ya nyama ya ng'ombe.

Alisema kuwa siku za kawaida bei ya nyama huwa ni shilingi elfu sita (6,000/-) kwa kilo, lakini katika kipindi hiki cha Noeli wafanyabiasha huwa na kawaida ya kupandisha bei ya bidhaa mbalimbali.

Aliongeza kuwa wafanyabiasha huwa na kawaida ya kuchanganya nyama na vitu vya ndani (ofals) kama vile utumbo, moyo na maini unaponunua nyama ya kawaida.

“Wauza nyama katika kipindi hiki wanakuwa na kuburi wanauza nyama wanavyotaka kuwa kujua kwamba watauza tu wanakuchanganishia na utumbo humohumo kwenye nyama ya kawaida,” alisema Elizabeth.

Naye mkazi wa kihesa katika Manispaa ya Iringa, Clementine Sambala alisema kuwa pamoja na kwamba hali ya maisha ni ngumu watu wamefurika katika mabucha kununua nyama ili kusherekea Krismasi.


Alisema krismasi ya mwaka huu imesuasua ukilinganisha na mwaka jana kila watu wanalia hali ngumu, biashara zao hazitoki na pia watu wengi hawana hela ya kununua mahitaji ya siku kuu ya krisma na mwaka mpya.

Mmoja wa wauza nyama ya ng'ombe anayeuliza nyama katika bucha iliyopo katika ya mji wa Iringa alipoongea na nipashe alisema kuwa wateja wanalifahamu hilo sio kitu kigeni.
Alisema kuwa kawaida siku kuu kama krismasi na mwaka mpya biashara huwa nzuri kwa hivyo huwa tunawachanganyia wateja nyama pamoja utumbo, na kuongeza kuwa hata siku kuu ya mwaka mpya itakuwa hivyohivyo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...