Skip to main content

RC MASENZA: VITENDO VYA UBAKAJI VISITOKEE TENA 2017








Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amani Juma Masenza akiongea na wananchi wa Mkoa wa Iringa kupitia vyombo vya habari kwa kuwatakia heri katika sherehe za Noeli na Mwaka Mpya 2017 leo ofisini kwake. (Picha na Friday Simbaya)




IRINGA: Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza amekemea vitendo vya ubakaji na ulawiti vinavyoendelea kujitokeza katika jamii na kuonya kwamba vitendo hivyo visitokee tena mwaka 2017. 


Mkuu mkoa huyo alisema hayo leo (Jumatatu) wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake, ambapo alitumia pia fursa ya kuwatakia wananchi wa Mkoa wa Iringa heri katika Noeli na Mwaka Mpya 2017.


Masenza ameviagiza vyombo vya dola vifanye kazi ya kuwabaini wahusika na kuwafikisha kwenye mkondo wa sheria.


Pia, mkuu huyo aliwaomba wananchi wa Mkoa wa Iringa kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vya ubakaji kwa watoto wadogo.


“Ni wajibu wetu sote kuhakikisha tunatokomeza kabisa vitendo vyote vinavyopelekea uvunjifu wa amani katika mkoa wetu wa Iringa na nchi kwa ujumla,” alisema Masenza.


Aidha, mkuu huyo aliwaomba wananchi wa Mkoa wa Iringa kwa umoja wahakikishe wanasimamia na kudumisha ulinzi na usalama ili mkoa uendelee kuwa na amani na utulivu.


“Napenda kuwatakia sikukuu njema ya Noeli na Mwaka Mpya 2017 wenye mafanikio tele. Ninawasihi kuhakikisha mnasherehekea sikukuu hizi kwa amani, usalama na utulivu,” alisema.


Alisema kuwa serikali itahakikisha ulinzi na usalama vinakuwepo kipindi chote cha sikukuu kwa sababu uzoefu unaonesha kuwa katika majira ya sikukuu watu wasiopenda kuona amani na utulivu wa mkoa hutumia majira haya kufanya uhalifu.


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza ni wa 21, tangu kuanzishwa kwa mkoa huu mwaka 1964, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Iringa alikuwa Philemon Muro (1964-1968).


Wakati huohuo, mkuu wa mkoa ametoa wito kwa wananchi kutumia vizuri mvua zinazoendelea kunyesha kwa kuhakikisha wanapanda mazao ili kujihakiishia uhakika wa chakula.


Alisema kuwa katika maeneo yanayopata mvua chache hususan Mahenge na Isimani wapande mazao yanayovumilia ukame.


Aidha, mkuu wa mkoa huyo aliwakumbusha wananchi kupanda miti katika msimu huu wa mvua kwa kuwa mkoa una hali ya hewa nzuri inayostawisha miti.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...