Skip to main content

TIGO YAZINDUA DUKA LA 'TEAM LEADERS' DEVIS CORNER TANDIKA TEMEKE




Msimamizi wa Biashara wa Kampuni ya Simu Tigo Dar es Salaam na Zanzibar, Nderingo Materu (wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka dogo la Tigo Tandika Devis Corner leo. Kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa Tigo Wilaya ya Temeke, Fadhila Saidi, Mwendeshaji wa duka hilo, Khadija Matambo na kushoto ni Meneja Huduma kwa Wateja wa kampuni hiyo, Isack Shoo.



Hawa ndio waendeshaji wa duka hilo. Kutoka kushoto ni Victor Juma, David Ngwale na kiongozi wao Khadija Matambo.



Meneja wa Tigo Uendeshaji wa huduma za Wateja , Isaack Shoo akihojiwa na wanahabari.



Picha ya pamoja.



Picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa duka hilo.




Na Dotto Mwaibale


KAMPUNI ya Tigo inayoongoza kwa maisha ya kidijitali Tanzania, leo imezindua rasmi mpangbo mdogo wa maduka ya huduma kwa wateja unaofahamika kama maduka ya Team Leaders ambayo yatatoa huduma za kampuni moja kwa moja kutoka maeneo wanayokaa wateja. 






Kwa mujibu wa Meneja wa Tigo Uendeshaji wa huduma za Wateja , Isaack Shoo maduka hayo kimsingi yatakuwepo katika maeneo ya makazi na yatatoa huduma zote za Tigo na miongoni mwake ni pamoja na kurudisha kadi za simu zilizopotea, mauzo ya muda wa maongezi, huduma za Tigo Pesa, mauzo ya kadi za Tigo na mauzo ya simu za kisasa (Smartphones).

Katika mkutano huo wa waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Shoo alisema, “Kupitia maduka ya team leaders Tigo imejikita kuhakikisha kuwa bidhaa zakehuduma zake zimo karibu na wateja, kuwezesha wateja wetu kufurahia huduma namba moja ambayo imo moja kwa moja katika kujikita kwetu katika mabadiliko ya kuboresha mtindo wa maisha ya kidijitali.”


Shoo alisema kuwa kila duka litakuwa na mawakala watano wa huduma kwa mteja ambao watakuwa wamepata mafunzo yanayohusiana na huduma kwa mteja kutoka Tigo ili kukidhi mahitaji ya wateja.


Aliongeza kuwa hadi sasa maduka yapo maduka matano ambayo yapo Mbande, Tandika, Tabata, Segerea na Ukonga (yote yapo Dar es Salaam) na tayari yanafanya kazi. 


Shoo aliongeza, “Maduka zaidi yanatarajiwa kuanzishwa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ambapo yatakuwa katika maeneo ya Kawe, Mawasiliano Towers, Kimara, Kigogo na Mwananyamala.”


Mbali na mafunzo Tigo pia itatoa vifaa muhimu kwa ajili ya biashara kwa mawakala wake katika hatua ya mwanzo ya kuanzisha biashara katika maduka, jambo ambalo ni muhimu na linalothibbitisha kujikita kwa kampuni hiyo ya simu katika kuisaidia serikali kstiks juhudi zake za kiupunguza ukosefu wa ajira nchini.


Hivi sasa Tigo ina maduka maduka makubwa 50 kwa ajili ya huduma kwa wateja yaliyoasambaa kote nchini yakiwa na uwezo wa kuhudumia wateja kati ya 200 na 300 kwa siku.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...