Skip to main content

WANAFUNZI 2,998 MANISPAA YA IRINGA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWA KWANZA 2017

Image result for iringa town pictures

Ufaulu wa wanafunzi waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi (PSLE) mwaka 2016 Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa umeongezeka ukilinganisha na mwaka jana, ambapo ufaulu kwa mwaka huu ni asilimia 87.43, wakati mwaka jana ulikuwa ni asilimia 85, sawa na ongezeko la asimilia 2.43.

Hayo yalisemwa na Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Mkoa (shule za msingi) Salimin Mndeme, jana wakati akiongea na SIMBAYABLOG kuhusu matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2016.

Alisema kuwa kuongezeka kwa ufaulu mwaka huu Manispaa ya Iringa ni kutokana na utekelezaji mzuri wa mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN) ulioanzishwa na serikali hivi karibuni, nakuongeza kuwa manispaa ya Iringa imeshika nafasi ya pili kimkoa (ya kwanza kimkoa ni Mafinga Mji).

Alisema kuwa wanafunzi waliofaulu mwaka 2016 ni 2,998 (1,414 wavulana na 1,584 wasichana) ambapo wanafunzi wote waliofaulu mwaka huu wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2017.

Alisema kuwa Manispaa ya Iringa ina jumla ya shule za msingi 50, lakini ni shule 48 kati ya hizo shule za serikali ni 42 na zisizo za serikali ni sita (6) ndio ambazo zilikuwa na wananfunzi waliofanya mtihani ya kumaliza elimu ya msingi.

Alisema kuwa wanafunzi watakaojiunga na elimu ya sekondari ni wale waliofaulu katika madaraja A, B na C ambaye jumla yake ni 2,998 wote watajiunga na elimu ya sekondari mwakani.

Aliongoza kuwa ufaulu umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka, kwa mfano, mwaka 2014 ufaulu ulikuwa ni asilimia 82.49, 2015 ufaulu ulikuwa asilimia 85 na mwaka huu ufauli ni asilimia 87.43.

Aidha, kaimu afisa elimu alisema kuwa jumla ya wanafunzi 3,440 (wavulana 1,624 na wasichana ni 1,816) waliosajiliwa kufanya mtihani lakini waliofanya mtihani huo ni 3,429 (wavulana 1,618 na wasichana 1,811) sawa na asilimia 99.7.

Katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi wanafunzi walitahiniwa katika masomo matano ambayo ni Kiswahili, maarifa ya jamii, kiingereza, hisabati na sayansi.

Aliongeza kuwa wanafunzi wengi walifanya vibaya katika masomo ya Kiingereza na Hisabati wakati masomo waliyofanya vizuri ni Kiswahili, Maarifa ya Jamii na Sayansi.

Hata hivyo, kaimu afisa elimu alisema kuwa Manispaa ya Iringa inaupungufu wa walimu wataalamu katika masomo ya Kingereza na Hisabati pengine ndio sababu za wanafunzi wengi  kufanya vibaya katika masomo hayo.

Alishauri kuwa ili kuongeza ufanisi katika utendaji kwa walimu serikali hainabudi kuwafanyia semina mara kwa mara yaani (in-service training) kwa walimu katika masomo ya kingereza na hisabati ili kuongeza ufanisi zaidi. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...