Skip to main content

ASKOFU MDEGELLA WA KKKT IRINGA AAGWA KWA KUZAWADIWA NYUMBA NA GARI


Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kusini, Isaya Mengele (kushoto) akimpongeza Askofu Dkt. Owdenburg Mdegella katika ibada maalum iliyofanyika katika usharika wa Kanisa Kuu (Cathedral) Iringa mjini leo. (Picha na Friday Simbaya)







KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa limemzawadia Askofu Dkt. Owdenburg Mdegella aliyemaliza muda wake wa uaskofu nyumba na gari vyenye thamani ya shilingi milioni 123. (123m/-).

Kanisa limeamua kumzawadia nyumba yenye thamani ya shilingi milioni 55/- iliyopo katika mtaa wa Kihesa-Kilolo Manispaa ya Iringa na gari aina ya Toyota Haice Pickup double cabin yenye thamani ya shilingi milioni 68/-.

Askofu Mdegella alizaliwa mwaka 1951 katika Kijiji cha Ipalamwa, Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa. 

Askofu huyo amekuwa askofu mkuu wa dayosisi ya Iringa ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kwa miaka 38 kama mchungaji, na miaka 30 kama askofu .

Askofu huyo ameagwa leo (jumatatu) katika ibada maalum ya kustaafu kwa heshima iliyofanyika katika usharika wa Kanisa Kuu (Cathedral) Iringa mjini, ibada ambayo ilihudhuriwa na Mkuu wa Kanisa la KKKT, Askofu Dkt. Fredrick Shoo.

Akisoma hati ya kustaafu kwa heshima askofu dkt owdenburg mdegella kwa niaba ya kanisa la KKKT, Katibu Mkuu wa KKKT- Dayosisi ya Iringa, Nayman Chavalla alisema kuwa Askofu Mdegella alichaguliwa na Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Dayosisi ya Iringa tarehe 8 Oktoba mwaka 1986 kuwa askofu kwa mujibu wa katiba ya dayosisi ya Iringa ya kanisa la KKKT.

Chavalla alisema kuwa kwa niaba ya washarika wote 142,000 wa dayosisi hiyo, askofu huyo amestaafu rasmi na kwa heshima.

Alisema kuwa Askofu Mdegella aliwekwa wakfu kuwa askofu na kuingizwa kazini kuwa mkuu wa dayosisi katika ibada iliyofanyika uwanja wa samora, mjini iringa tarehe 27 januari, 1987.

Kwa upande wake, Askofu mstaafu Dkt. Mdegella kwa niaba ya Dayosisi ya Iringa amewapongeza washarika kwa zawadi na kumshukuru Mungu kwa utumishi wake.

Alisema kuwa kama mchungaji mara nyingi alikumbana na uasi, kupingwa, na kutishiwa maisha yake alipokuwa akitetea kweli ya injili, lakini kwa nguvu za Mwenyezi Mungu alishinda changamoto hizo.


Ibada maalum ya kustaafu kwa heshima Baba Askofu Dkt. Owdenburg Mdegella ilihudhuria na wageni mbalimbali kutoka Ujerumani, Sweden na Marekani pamoja na viongozi wa serikali ya mkoa wa Iringa na viongozi wa siasa na washarika wa Dayosisi ya Iringa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...