Skip to main content

CCM IRINGA YAZINDUA SHEREHE ZA KUADHIMISHA MIAKA 40



Na Friday Simbaya, Iringa

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu amewashukuru wazee wasisi wa chama hicho kwa kukijenga imara na misingi bora. 

Alisema kuwa CCM ina misingi bora na kinawajali wananchi, na kuongeza kuwa pasipo kuwa na wazee hao chama kisingejenga misingi imara.

Msambatavangu ambaye alikuwa mgeni rasmi alitoa kauli hiyo juzi wakati wa uzinduzi wa sherehe za kutimiza miaka 40 ya CCM zinatarajiwa kuadhimishiwa Dodoma tarehe 5 Februari mwaka huu, ambapo zitaadhimishwa kwa mikutano ya ndani na makongamano.

Mwenyekiti huyo amepongeza misingi bora iliyojenga na viongozi hao kwa kuachiana madaraka kwa utaratibu mzuri.

Akitoa mfano wa Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kuongoza taifa hili na baadae kumuachia Mzee Mwinyi naye kumuachia Benjamin Mkapa na Mkapa kumuachia Jakaya Kikwete na kikwete kumkabidhi nchi Dkt. John Magufuli.

“Hiyo yote ni misingi bora na imara iliyojengwa na viongozi wasisi wa taifa hili. Ni bora kuenzi amani iliyopo kwa manufaa na ustawi wa nchi.,” alisema.

Aidha, Msabatavangu alionesha kukelwa na vitendo vya ubakaji kila kukicha ambapo watoto wadogo wanabakwa, jambo ambalo ametakalikema mara moja.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini, Abed Kiponza amewashukuru wananchi wote wa Mkoa wa Iringa kwa uvumilivu wao wanaoonesha pamoja na kupoteza Jimbo la Iringa mjini.

Jimbo hilo kwa sasa linaloongozwa na Mchungaji Peter Msigwa kupitia CHADEMA, na kuwataka wananchi kuendelea kuwavumilia wakati huu chama kikuendelea kujiimarisha katika chaguzi zijazo.

Kiponza alisema kuwa wakati sherehe kutafanyika shughuli mbalimbali ambapo kata za Kigamboni na Kitwiru mjini Iringa zitajengwa ofisi za kata katika maeneo hayo, na tayari ujenzi unaendelea. 

Vilevile amewataka viongozi mkoani Iringa kuwahimiza wanachama katika maeneo yao na kuwakumbusha kulipa ada ya uanachama.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Wilaya ya Iringa mjini, Nuru Ngereja alisema kuwa katika miaka 40 ya maadhimisho, chama kimepanga kutembelea vituo vya kulelea watoto yatima ikiwepo Hospitali ya Manispaa ya Frelimo.

Hata hivyo alisema kuwa lengo la kuundwa Chama cha Mapinduzi ni kuendeleza harakati zilizokuwa zikifanywa na vyama vya ASP na TANU za kuwaletea maendeleo Watanzania kwa haraka bila ya ubaguzi wa aina yoyote nchini kwani ndivyo vyama zilivyoleta ukombozi.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela amewataka wenyeviti wa CCM na kata kutoa taarifa za maendeleo ya kata ili kurandana kasi ya Magufuli ya ‘hapa kazi tu.’

Kasesela aliomba viongozi hao wanaCCM kujitahidi kuhimiza usafi wa mazingira katika maeneo yao, ili kutimiza lengo la usafi wa kila mwisho wa mwezi.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...