Skip to main content

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI LATOA WITO KWA WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO



Kamanda wa Jeshi la Zimamoto mkoani Iringa Kennedy Komba akizungumza na Nipashe katika mahojiano maalum kuhusu mikakati iliyowekwa na jeshi hilo kupambana na majanga ya moto mkoani Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya) 




Na Friday Simbaya, Iringa 

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Iringa Mrakibu kennedy Komba ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa askari wanaokuwepo kwenye eneo la tukio. 

Alisema kuwa wananchi wanaokuwepo eneo la tukio huchelewa kutoa taarifa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutokana na kuanza kwanza kuokoa mali zilizomo ndani ya Jengo linaloungua bila kutoa taarifa kwanza kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. 

Mrakibu huyo alitoa kauli hiyo wakati wa mahojiano maalum na nipashe ofisini kwake jana na kuongeza kuwa wananchi wanabudi kutoa ushrikiano kwanza ili askari waweze kuokoa mali, hasa katika majanga ya moto. 

Alisema kuwa ujenzi holela na uwekwaji wa vikwazo kama vile matairi chakavu, kanopi, vyuma na mawe makubwa kando ya mitaa finyu ya maeneo hayo ni sababu mojawapo zinazochelewesha zoezi la kuoaji. 

Katika hatua nyingine, Mrakibu Kennedy Komba amewata wananchi na makapuni kuleta mchoro yao ya nyumba kwa jeshi hilo ili wawezo kuelekezwa sehemu ya kuweka vifaa vya moto. 

Kamanda huyo amewataka wamiliki wa majengo na nyumba mkoani Iringa kuhakikisha wanafunga vifaa vya zima moto ili kujiadhari na majanga ya moto mara yanapotokea. 

Komba alisema katika kuuweka mkoa wa Iringa salama na janga la moto, jeshi la zimamoto linaendelea kutoa elimu na mafunzo kwa umma ili kuaondoa tatizo la janga la moto. 

Alisema lengo la mafunzo na elimu hiyo ni kuwapa uelewa jinsi ya kuepukana na majanga ya moto katika jamii. 



Kamanda alisema vifaa vinavyotakiwa kuweka katika majengo na nyumba kwa ajili ya kujikinga na majanga ya moto ni pamoja na ndoo ya mchanga mkavu, Fire Extingusher pamoja na viashiria vinavyotoa sauti kama king’ola. 

Aidha Komba amesihi wamiliki wa vyombo vya usafiri na usafirishaji kuhakikisha wanapeleka vyombo vyao kufanyiwa ukaguzi na kupewa fomu maalum ya ukaguzi, na kununua vifaa vya kudhibiti janga hilo ili kuondokana na athari. 

Hata hivyo, kamanda huyo jeshi la zimamoto na uokoaji amewataka wananchi kutotumia namba ya dharura 114 kutoa taarifa za uongo kwa jeshi hilo badala yake watumie vizuri kwa kutoa taarifa zitakazofanya jeshi kufika haraka kwenye matukio hayo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...