Skip to main content

TRA MKOA WA IRINGA KUKUSANYA ZAIDI YA 63BN/- MWAKA 2016/17



Mamlaka ya Mapato Manzania (TRA) mkoani Iringa imepangiwa lengo lakukusanya mapato ya shilingi 63bn/- katika mwaka wa fedha 2016/2017, amesema Charles Kichere Naibu Kamishna Mkuu wa TRA.

Kichere alisema hayo wakati mkutano wa TRA na wafanyabiashara kutoka mikoa ya Njombe na Iringa uliofanyika mkoani Iringa juzi.

Alisema kuwa mkoa wa iringa ukiwa ni mmoja ya mikoa tajiri nchini itakusanya mapato hayo kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato.

Kichere alisema kuwa mapato hayo yatakusanywa kutoka kwa wafanyabiashara, walipa kodi, waajiri, makandarasi pamoja na wadau wengine wa kodi.

“Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imeendelea kubuni mikakati mbali mbali ya kuongeza ukusanyaji wa mapato ili kuendana na kauli mbiu ya serikali ya awamu ya tano isemayo “HAPA KAZI TU” ili kutimiza na kuvuka lengo la kukusanya shilingi trilioni 15.1 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17,” alisema Kichere.

Alisema hivi sasa nchini inaelekea katika uchumi wa kati na wa viwanda hakunabudi kutimiza lengo la kuifanya bajeti ya taifa kujitegemea kwa kiwango kikubwa. 

Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha bajeti ya shilingi trilioni 29.5 ya mwaka wa fedha 2016/17 ambayo iliwasilishwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango June 08, 2016.

Bajeti hiyo ilipigiwa kura na wabunge waliokuwepo bungeni, ambapo jumla ya wabunge 251 walipiga kura za ndio za kuipitisha bajeti hiyo kati ya wabunge 252 waliokuwepo ukumbini wakati kura hizo zikipigwa.

Katika hatua nyingine, Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kichere amewashauri wafanyabiashara nchini kutumia mashine za kielectroniki (EFDs) kwani kutasaidia kukuza pato la Taifa.

Naye, Onesmo Mwajombe mfanyabiashara kutoka mkoa wa Njombe aliomba serikali kupeleka hela kwenye mabenki ili waweze kukopa, ambapo aliongeza kuwa mitaji yao iko taabani.

Alisema kuwa ili serikali iweze kukusanya mapato kutoka kwa wafanyabiashara hainabudi kupeleka fedha kwenye mabenki ili wafanyabiashara waweze kukopa kwa ajili kuimarisha mitaji.

“Tukiende kwenye mabenki kukopa fedha ya mitaji tunaambiwa wapo kwenye kipindi cha mpito…, ” alisema Mwajombe.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...