Skip to main content

VIJANA NCHINI WAASWA KUJITUMA NA SIO KUKAA BURE…






Bwana John Massao na Theresia Massao wakiwa katika mmoja ya mizinga walioweka katika msitu wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa eneo la Gangilonga, mkoani Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya)





IRINGA: VIJANA nchini wanatakiwa kujishughulisha na ufugaji wa nyuki kisha kujikwamua kimaisha kwa kuongeza kipato, kiuchumi kuliko kutegemea serikali kuwatafutia ajira.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Mkurugenzi wa TEJO’s Honey, John Massao jana wakati akiongea na nipashe, ambao niwazalishaji na wasindikaji wa asali asilia mjini iringa. 

Massao alisema kuwa vijana ndio kundi kubwa lisilokuwa na ajira wala mapato katika mfumo wa maisha na wanahitaji kujiajiri kwa kutumia rasilimali na maliasili zilizoko katika mazingira yao.

Aliwataka vijana hao kujiunga kwenye vikundi vya pamoja na kuanzisha ufugaji wa nyuki na kuweza kupata asali na nta kisha kupata soko litakalosaidia kujiinua kiuchumi na kuongeza mapato katika familia ikiwa ni pamoja na kuepukana na kujihusisha na vitendo vya uhalifu kwa kuvunja sheria. 

Alisema kuwa vijana wasisubiri ajira za maofisini tu kumbe wange tumia rasilimali ya misitu kufuga nyuki kuliko kubaki maisha tegemezi na ombaomba kumbe wangeweza kutumia ardhi na misitu ya asili jirani na hifadhi za Taifa.

“Nchi hii ina mapori mengi lakini vijana wakijiunga kwa pamoja kwa kuweka mizinga katika mapori ambayo utasaidia kuhifadhi misitu na mioto,” alisema Massao.

Alisema kuwa asali ikivunwa inadumu kwa muda mrefu mpaka miaka 100 na haiitaji kupaliliwa wa kuweka mbolea kama shambani, kwa hiyo vijana watumia fursa waingie katika soko la ufugaji.

Awali Mkurugenzi wa TEJO’s Honey, Theresia Massao aliitaka serikali na wadau mbalimbali kuhamasisha jamii kufuga nyuki kwa kutumia njia za kisasa na kuzalisha kwa wingi zao hilo .

Theresia alisema takwimu inaonesha Tanzania ina misitu mingi ambazo ni makazi ya makundi ya nyuki na ikitumika vizuri na vijana kufugia nyuki kwa kuzalisha asali itainua kipato cha mwananchi mmoja mmoja.

“Kutokana na ufugaji wa nyuki jamii inaweza kujipatia gundi ya nyuki , sumu ya nyuki inayotumika katika tiba pamoja na maziwa ya nyuki kama chakula na tiba “alisema Theresia.

Vilevile alifafanua kuwa wananchi kwa kufuga nyuki wataweza kuboresha afya za familia kwa sababu asali inatumika kama chakula na tiba kwa magonjwa mbalimbali kama vile vidonda vya tumbo na kansa.

Katika hatua nyingine aliwaasa wananchi na wafugaji kujiepusha na uharibifu wa mazingira kwa kuchoma na kukata miti na makazi ya nyuki kwa kukosa maua na maji kisha kuzalisha kiwango kidogo cha asali na nta na hata kuhama katika mizinga baada ya kupata usumbufu wa makazi kimazingira.

TEJO ni muuganiko wa majina mawili yaani, Theresia na John (TEJO) ambao ni mume na mke walieamua kuanzisha kampuni hiyo baada ya kustaafu utumishi wa umma kama maofisa misitu.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...