Skip to main content

WANAFUNZI 17,549 KUJIUNGA NA ELIMU YA SEKONDARI MKOANI IRINGA

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu (kushoto) ambaye pia ni Katibu wa Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa (RCC) akisoma taarifa katika kikao hicho huku Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza ambaye pia mwenyekiti wa kikao hicho akifuatilia kwa makini leo. 







Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Suzana Mgonukulima (CHADEMA) na Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini, Menrad Kigola (CCM) wakibadilishana mawazo nje ya Ukumbi wa Siasa ni Kilimo wakati wa Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa wa Iringa (RCC kilichofanyika leo  (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)





IRINGA: Jumla la wanafunzi 17,549 mkoani Iringa (wavulana 7,988 na wasichana 9,561) sawa na mkiondo 439 watajiunga kidato cha kwanza mwaka 2017, imeelezwa.

Hayo yalisemwa na Kaimu Afisa Elimu wa Mkoa wa Iringa Richard Mfugale (pichani) wakati wa Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa (RCC) kilichofanyika leo mjini Iringa.

Kaimu afisa elimu huyo alisema kuwa wanafunzi wote waliofauli wamechaguliwa kujiunga elimu ya sekondari mkoani iringa, ambapo aliongeza kuwa halmashauri zote zinaendelea na maandalizi ya kupokea wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza.

Mfugale alisema kuwa ufaulu wa mtihani wa kidato cha nne kimkoa umepanda kutoka asilimia 65.25 mwaka 2013 hadi asilimia 72.34 mwaka 2015, hali kadhalika kwa halmashauri ya manispaa ya iringa na halmashauri ya wilaya ya iringa ufaulu umekuwq ukiongezeka. 

Kwa upande wa mtihani wa kidato cha sita, Mfugale alifafanua kuwa kati ya wanafunzi 4,142 waliohitmu kidato hicho, wanafunzi 4,055 sawa na asilimia 97.88 ya walifauli kwa kiwango cha daraja la kwanza hadi la nne.

Alifafanua kuwa kati yao hao waliofauli asilimia 95.6 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu wamechaguliwa kujiunga na vyuo vikuu na vyuo vingine nchini.

Wakati huohuo, mjumbe wa kikao hicho, Mendrad Kigola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini alisema kuwa ili kuwepo boreshaji elimu, halmashauri za wilaya hazinabudi ya kutenga kiasa cha pesa kutoka katika kwenye bajeti zao kwa ajili ya maendeleo ya elimu.

Alisema kuwa ili kuunga juhudi za serikali katika sera yake ya elimu bure ni lazima halmashauri zitoe mchango wake.

Aidha, mjumbe huyo alishauri pia kuwa kuwepo na jitihadi za makusudi mazima za kutoa elimu kwa wazazi na walezi kuhusu elime bure ili kupunguza malalamiko na mkanganyiko uliopo wa suala la sera ya elimu bure.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...