Skip to main content

DC MUWANGO AIAMURU HALMASHAURI YA WILAYA YA NACHINGWEA KUREJESHA ARDHI YALIYOVAMIWA



Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango akisisitiza umuhimu wa kufanya mazoezi


Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango akionyesha mfano wa ufanayaji mazoezi


Mkuu wa wilaya ya Nachingwea ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya hiyo Mhe Rukia Muwango akifanya mazoezi katika uzinduzi huo

Matembezi yakiendelea vyema

Na Mathias Canal, Lindi

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango ameitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo irejeshe maeneo yote ya wazi yaliyo vamiwa na kutumika kinyume cha matumizi yaliyolengwa.

Dc Muwango ametoa agizo hilo mjini Nachingwea kwenye uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasioambukiza na yanayoweza kuzuilika kupitia mazoezi na michezo.

Uzinduzi huo uliofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine ambapo Alisema kuwa yeye kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo anatambua na anazotaarifa za kutosha kuwa maeneo mengi ambayo yalitengwa kwa ajili michezo na shuguli nyingine za umma yamevamiwa na kubadilishwa matumizi.

Dc Muwango ameitaka halmashauri hiyo kurejesha haraka kutoka mikononi mwa wavamizi.

Katika hali inayoonesha kuwa mkuu huyo wa Wilaya amelivalia njuga suala hilo, ameitaka Halmashauri hiyo ipeleke na kumkabidhi mikakati na taarifa za utekelezaji wa agizo lake haraka iwezekanavyo.

Sambamba na agizo hilo Muwango ameitaka Halmashauri hiyo kutenga maeneo kwa ajili ya michezo.

Amebainisha kuwa bila kuwa na maeneo ya wazi itakuwa vigumu kufanikiwa kukuza michezo na kuibua vipaji mbalimbali vya wanamichezo.

Amemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kuwaandikia wakuu wa shule za sekondari na walimu wakuu wa shule za msingi ili warejeshe mbio za mchakamchaka kwenye shule zao kwani shule nyingi wanafunzi hawakimbii mchakamchaka.

"Jambo ambalo ni muhimu kwa afya na akili za wanafunz ila walimu wawe na usimamizi mzuri ili wanafunzi wasiathiriwe katika masomo na usalama wao," Alisistiza Muwango.

Akizungumzia umuhimu wa michezo na mazoezi Dc Muwango alisema kuwa licha ya kuimarisha, umoja,undugu na mshikamano.
Lakini pia mazoezi na michezo ni kichocheo kikubwa cha maendeleo, utulivu na amani katika jamii.

Alibainisha kuwa chanzo cha baadhi ya migogoro katika baadhi ya jamii ni magonjwa ambayo yanaweza kuepukwa kwa kufanya mazoezi ambapo Hata hivyo jamii husika hazitambui jbo hilo Badala yake inayahusisha magonjwa hayo na sababu zisizo na msingi Ikiwa ni pamoja na Imani potofu, uchawi na ushirikina mambo ambayo hupelekea kunyoosheana vidole na kusababisha migogoro.

"Lakini mtu akiwa mgonjwa hawezi kufanya shuguli za kiuchumi na maendeleo yake mwenyewe, Taifa na hata wanaomuuguza hawawezi kufanya kazi ambazo zingewaletea maendeleo," Aliongeza Muwango.

Mkuu huyo wa Wilaya alitoa wito kwa wananchi wilayani humo kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi bila kujali rika Huku akiwaasa kuunda vikundi vya michezo na mazoezi Kwa sababu madhara ya kutofanya mazoezi ni makubwa ambapo sio rahisi kuyabaini haraka.

Uzinduzi huo ambao ni utekelezaji wa agizo la makamu wa Rais aliyetaka kuwe na kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasioambukiza na yanayozuilika kupitia michezo uliandaliwa na ofisi ya mkuu huyo wa wilaya ya Nachingwea Ambapo michezo mbalimbali ilichezwa, sambamba na upimaji wa afya na uchangiaji damu kwa hiari.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...