Skip to main content

DC WASHUKIA VIJANA WANAOCHEZA KAMARI ‘KUBETI’

DC KASESELA

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela amewata vijana nchini kuachana na tabia ya kucheza kamari yaani ‘kubeti’ kwa kutabiri mambo kadhaa.

Hapa Tanzania mchezo maarufu ni soka, hivyo mashabiki wa mchezo huo utabiri mambo kadhaa katika mchezo husika, ikiwemo wafungaji wa magoli, idadi ya magoli kwenye mechi husika, magoli yakufungwa kipindi kipi cha mchezo na ukuisha matokeo yatakuwaje.

Kasesela alisema kuwa vijana watakiwa kujishughulisha na shughuli za kiuchumi na kuachana mazoea kutengenza pesa kwa njia mikato kama kucheza kamari.

Akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya Kombe la J.Msofu na kukabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza na wa pili, Kasesela alizipongeza timu hizo kwa kucheza mchezo mzuri huku akiwataka wachezaji kucheza mpira kwa kuwa mpira ni ajira.

Timu ya Itengulinyi FC iliyopo kwenye kata ya Maboga ilitwaa ubingwa baada yakuichakaza timu ya Kiponzelo FC kwa mabao 4-3 kwa mikwaju ya penalti kwenye mashindano ya kombe la Msofu Cup yaliyomalizika hivi karibuni.

Mechi hiyo ya fainali kati ya timu hizo mbili uliyochezwa katika uwanja wa shule ya sekondari kiponzelo, kata ya maboga na tarafa ya kipozelo, wilayani Iringa.

Mechi hiyo ya fainali kati ya timu hizo mbili uliyochezwa katika uwanja wa shule ya sekondari kiponzelo, kata ya maboga na tarafa ya kipozelo, wilayani Iringa.

Kwa upande wake, mdhamini wa mashindano hayo Jeremia Msofu alisema kuwa lengo la mashidano hayo nikuibua vipaji vitakavyoweza kuunda timu ya Jimbo la Kalenga, itakayoweza kucheza kuanzia Ligi ya daraja la nne la hadi Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Mashindano hayo yalianza rasmi decemba 11 mwaka jana na kumalizika Februari 5 mwaka 2017.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza na wa pili mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela alizipongeza timu hizo kwa kucheza mchezo mzuri huku akiwataka wachezaji kucheza mpira kwa kuwa mpira ni ajira.

Mshindi wa kwanza alizawadiwa ng’ombe mmoja mwenye thamani ya 500,000 na mshindi wa pili mbuzi wawili wenye thamani ya 150,000/-.

Hata Golikipa bora katika mashindano hayo Adam Jaffari alizawadiwa fedha taslim 50,000/-, mfungaji bora akizawadiwa 50,000/- huku timu yenye nidhamu katika mashindano hayo yaani Usengelindete ikiondoka na zawadi ya 50,000/-.

Mashindano hayo yalizinduliwa rasmi na Katibu wa Chama cha Mpira Iringa Vijijini ,Juma Lalika, ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya uchaguzi wa Chama cha Mpira Tanzania (TFF).

MWISHO



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...