Skip to main content

MKOA WA IRINGA KUZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI




KATIBU Tawala wa Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu amesema katika maadhimisho ya Siku ya wanawake watazindua Jukwaa la uwezeshaji wanawake Kiuchumi Kimkoa ambapo washiriki ni wawakilishi wa Vikundi vya Wanawake kutoka katika Halmashauri zote za Mkoa.

Alisema kuwa wanawake na jamii kwa ujumla wajitokeza kwa wingi kushiriki katika maadhimisho ya Siku ya wanawake ili kujumuika na wanawake wengine kubadilishana mawazo na kupeana uzoefu wa masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

Aidha, Wamoja anaomba wadau mbalimbali kujitokeza kutoa huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu ya ujasiliamali na kuelezea fursa zilizopo kwa wanawake kama Mchango wao katika maadhimisho haya.

Alisema kuwa lengo la Jukwaa ni kuwaweka Wanawake pamoja ili waweze kutambua na kujadili fursa zilizopo katika maeneo yao na kuweka mikakati ya namna ya kuzitumia kwa maendeleo.

“Huu ni utekelezaji wa Maelekezo ya Serikali kupitia baraza la uwezeshaji Wanawake Kiuchumi. Baada ya uzinduzi huo kwa ngazi ya Mkoa, utafanyika pia uzinduzi katika kila Halmashauri,” alisema Wamoja.

Tarehe 8 Machi, kila mwaka siku ya wanawake Duniani huadhimishwa ikiwa ni muitikio wa Azimio la Umoja wa Mataifa.

Tanzania ikiwa ni Mwanachama wa Umoja wa Mataifa inaungana na Mataifa mengine kuadhimisha siku hiyo.

Lengo la kufanya maadhimisho hayo ni kutambua na kuheshimu mchango wa Wanawake katika maendeleo ya Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii na kutoa fursa kwa Wanawake kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo yao.

Maadhimisho ya mwaka huu 2017, yataongozwa na kaulimbiu isemayo; TANZANIA YA VIWANDA, WANAWAKE NI MSINGI WA MABADILIKO YA KIUCHUMI.

Kauli mbiu hii inakwenda sambamba na mipango na Sera za nchi zinazolenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.

Vilevile, anapenda kuikumbusha jamii kwamba wanawake wana mchango mkubwa katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda, hivyo kuna haja ya kuwapa nafasi ya kutosha katika kushiriki katika kuendeleza viwanda.

“Sote tutambue kwamba viwanda vinaharakisha maendeleo na mabadiliko ya kiuchumi katika jamii. Na umuhimu wake mkubwa unaonekana katika kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa na wananchi,” alisema.

Alisema kuwa kwa wanawake ndiyo kundi kubwa linalojishughulisha na kilimo uwepo wa viwanda ni muhimu sana kwa kuwa utawasaidia katika kuongeza thamani mazao mbalimbali wanayozalisha.

Viwanda vilevile, vitawawezesha kupata nyenzo za kurahisisha kupunguza mzigo wa kazi unaowaelemea wanawake.

Kutokana na mnyororo huu, uwepo wa viwanda utawawezesha wanawake kutoa mchango wao zaidi katika kujiletea maendeleo ya kiuchumi wao wenyewe, familia zao na maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Wakati huohuo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu alitumie fursa kutoa wito kwa Wanawake katika Utumishi wa Umma kutumia fursa mbalimbali zilizopo kujiendeleza kielimu ili kujiongezea uelewa zaidi.

Fursa zipo nyingi kupitia Nchi mbalimbali ambazo zinatoa ufadhili wa masomo ya Uzamili na kutumia elimu hiyo kusaidia Wanawake wengine kwenye maeneo yao ya kazi kupitia huduma wanazozitoa, lakini pia kusaidia kujenga uwezo wa Wanawake wengine walio nje ya Utumishi wa Umma ambao ni kundi kubwa sana na wengi wao wakijishughulisha na shughuli mbalimbali za kukuza kipato na kujiletea maendeleo yao.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...