Skip to main content

TUNDU LISSU MAHAKAMA YA KISUTU KESI YA UCHOCHEZI




Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, amemtaka Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Salum Hamdani, kueleza anachofahamu juu ya Katiba ya Zanzibar na kama Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar , Salum Jecha ana mamlaka ya kufuta matokeo ya uchaguzi au laa.


Lissu alihoji hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati Hamdani alipokuwa akitoa ushahidi katika kesi ya uchochozi inayomkabili Lissu na wahariri wa Gazeti la Mawio.


Mshtakiwa Lissu aliomba kujiwakilisha mwenyewe mahakamani hivyo baada ya ushahidi alimuhoji maswali shahidi kulingana na ushahidi wake.


Swali hilo la Lissu lilimfanya Wakili wa Serikali, Paul Kadushi, kupinga akitaka shahidi asijibu kwa sababu si mtaalamu wa sheria wala Katiba.


Kadushi alidai shahidi hawezi kutoa tafsiri ya Katiba ya Zanzibar na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza masuala ya kikatiba.


Akijibu pingamizi hilo, Lissu alidai halina msingi wowote kwa sababu suala la Serikali ya Zanzibar ni halali na limeletwa na upande wa mashtaka wenyewe katika shtaka la pili na la tatu hivyo wakabiliane nalo.


Wakili Peter Kibatala alidai mahakamani hapo kuwa shahidi huyo anapaswa kueleza yeye mwenyewe kama hawezi kulijibu swali hilo na si vinginevyo na kwamba katika kuandika uamuzi wake mahakama ipende isipende ni lazima itajibu swali hilo.


Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili aliahidi kutoa uamuzi leo iwapo shahidi aeleze anachokifahamu kuhusu Katiba ya Zanzibar ama la.


Kabla ya kufikia katika malumbano hayo Lissu alitaka kujua yeye na washtakiwa wenzake walikula wapi kuchapisha huo uchochezi.


Alihoji wao watu wanne waliwasiliana kwa maandishi, email ama simu na saa ngapi, maswali hayo yalijibiwa na shahidi kwamba hafahamu.


Awali akihojiwa na Wakili Kibatala kuhusu wapi alipata taarifa za kuwapo kwa mikusanyiko ya watu katika sehemu za kuuzia magazeti , Hamdani alidai alizipata kwa RCO wa Kinondoni, Temeke na Ilala na kwa upande wa Zanzibar alipata kutoka kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Diwani Athumani.


Shahidi alidai katika Gazeti la Mawio la Januari 14 mpaka 20 kulikuwa na habari yenye kichwa cha habari Machafuko yaja Zanzibar na kwamba maneno hayo yangeweza kuleta chuki, uvunjifu wa amani, uchochezi na hofu.


Alidai baada ya kuona hivyo na kulinua gazeti hilo alifungua jalada la uchunguzi kisha aliteua wapelelezi ili kuona kama kuna kesi ya jinai na walipoona waliwafikisha washtakiwa mahakamani.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...