Skip to main content

Umoja wa Ulaya watoa Bilioni 22 kusaidia mradi wa Lishe na Usalama wa Chakula


Katika kusaidia Tanzania kuwa moja ya nchi ambazo wananchi wake wana lishe salama, Umoja wa Ulaya (EU) umechangia Euro milioni 9.5 (Tsh. 22 Bilioni) kwa ajili ya kusaidia kutekelezwa kwa mradi wa Lishe na Usalama wa Chakula unaotekelezwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) wenye thamani ya Euro milioni 24.5 (Tsh. 57.7 bilioni) unaotarajiwa kufanyika katika mikoa ya kanda ya kati. Akizungumza kuhusu msaada huo, Mkuu wa Ubalozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Roeland Van De Geer alisema EU imeamua kusaidia jamii ya Tanzania kupata lishe bora kwani wao wanaamini kuwa pasipo lishe bora mambo mengi ambayo yanahusu maendeleo ya taifa hayawezi kufanyika kwa kasi ambayo yanatakiwa kwenda nayo lakini pia mpango wa kusaidia lishe salama ni moja ya mambo ambayo EU imepanga kusaidia. 

Mkuu wa Ubalozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Roeland Van De Geer akizungumza kuhusu mchango wa Euro milioni 9.5 (Tsh. 22 Bilioni) kwa ajili ya kusaidia kutekelezwa kwa mradi wa Lishe na Usalama wa Chakula wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP). (Picha zote na Rabi Hume)

“Kupitia mradi huu EU pamoja na WFP ziko katika nafasi nzuri ya kubaini na kuunga mkono uhusiano katika kilimo, afya, usalama wa chakula na lishe ambao hapo kabla haukuwa umeelezwa kwa kina na kufuatiliwa kikamilifu, matumaini yetu ni kuwa viongozi na wananchi kwa pamoja wataungana kufanikisha mradi huu,” alisema Van De Geer. Nae Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), Michael Dunford aliishukuru EU kwa kutoa msaada ambao utawezesha jamii ya Tanzania katika mikoa wa Dodoma na Singida kusaidiwa kupata lishe salama ikiwa ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo Endelevu (SDGs). 

Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), Michael Dunford akizungumza kuhusu mradi wa Lishe na Usalama wa Chakula.

“Tunashukuru kwa mchango huu kutoka Umoja wa Ulaya kwani umeiwezesha WFP kuendelea na programu hii bunifu inayolenga kukidhi mahitaji ya watu walio hatarini zaidi na hasa watoto katika kipindi cha ukuaji wao” alisema Dunford. Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubisya alisema mradi huo utafanyika kwa mikoa miwili ya Dodoma na Singida ambapo takwimu za kudumaa kitaifa ni aslimia 34 na Dodoma ni asilimia 34 na Singida ni 36.5 na utafanyika kwa miaka mitano. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubisya akielezea jinsi mradi wa Lishe na Usalama wa Chakula utakavyofanyika nchini, takwimu za kudumaa na mikoa ambayo utafanyika.

Aidha Dk. Ulisubisya alisema uwekezaji huo wa WFP utahusisha kuwapa chakula, kutoa elimu jinsi ya kuzalisha vyakula vya aina mbalimbali, kuwawezesha kuwa na wanyama, jinsi ya kuwa na mazao ya kuuza na walengwa wakubwa ni kina mama wajawazito na watoto. 

Mkuu wa Ubalozi wa Umoja wa Ulaya nchini, Roeland Van De Geer na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), Michael Dunford wakisaini makubaliano ya Umoja wa Ulaya (EU) kutoa mchango wa Euro milioni 9.5 (Tsh. 22 Bilioni) kwa ajili ya kusaidia kutekelezwa kwa mradi wa Lishe na Usalama wa Chakula.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...