Skip to main content

WAJASIRIAMALI WASHAULIWA KUJIUNGA MFUKO WA BIMA YA AFYA

Kaimu Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Iringa, Lucas Gama akiongea na Nipashe jana. (Picha na Friday Simbaya)


Wajasiriamali washauliwa kuunda vikundi ili waweze kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na hatimae waweze kurahisisha upatikanaji wa matibabu pindi wanapoenda hospitali kutibiwa.

Akizungumza na Nipashe jana Kaimu Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Iringa, Lucas Gama alisema kuwa watu wasio watumishi wa serikali wanaruhusiwa kujiunga na mfuko wa bima ya afya kupitia vikundi vya ujasiriamali. 

Alisema kuwa wajasiriamali toka vikundi mbalimbali mkoani Iringa wamehamasishwa kujiunga na mfuko wa NHIF, ili kurahisisha matibabu wawapo katika shughuli zao za kawaida, na kuongeza kuwa wajasiriamali watakaojiunga na mfuko huo na kuwa wanachama watalipia shilingi 76,800/- kila mmoja.

Gama alisema kuwa mfuko wa NHIF ni mfuko wa kijamii unayotumia dhana ya ‘mshikamano wa kijamii’ kwa maana ya kuwa wanachama wote ni sawa mbele ya jamii, yaani, mchangiaji mdogo na anayechangia hela kubwa wote ni sawa.

Alisema kuwa majukumu ya NHIF ni pamoja na kuhakikisha vituo vya kutolea huduma za afya zinajitosheleza kwa kuwa na mahitaji yote muhimu kwa kutoa huduma bora kwa wanachama wake.

“Kwa kweli ugonjwa hauna siku wala hodi ni vizuri mtu ukajiandaa kwa maisha ya baadaye kwa kujiunga na mfuko wa bima ya afya…,” alisema Gama.

Alisema kuwa mfuko wa bima ya afya umejipanga kuhakikisha mwanachama anapata matibabu stahiki kwa kutumia kadi zao za bima kwa kuwa gharama zote za matibabu zimelipiwa na mfuko.

Akizungumzia uhaba wa dawa katika vituo vya afya na hospitali ambazo zimeteuliwa kutoa matibabu kwa kupitia mfuko huo, alisema kuwa, tatizo la ukosefu wa dawa hospitalini litamalizika, endapo kaya nyingi zitajiunga na mfuko wa NHIF, kwani serikali nayo itaweka mkono wake ili kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa.

‘’Tunahamasisha na kutoa Elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kujiunga na mfuko wa bima ya Afya makanisani, misikitini, kwa waendesha pikipiki (bodaboda), kwa viongozi wa dini na jamii kwa ujumla’’alisema Gama.



MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...